Home » » STAMICO YACHANGIA MILIONI 20 MAAFA YA TETEMEKO LA ARDHI KAGERA

STAMICO YACHANGIA MILIONI 20 MAAFA YA TETEMEKO LA ARDHI KAGERA

01
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akizungumza na wawakilishi wa Taasisi mashirika mbalimbali (Hawapo pichani) zilizochangia wanananchi wa Bukoba Mkoani Kagera waliopatwa na maafa ya tetemeko la ArdhiSeptemba 10 mwaka huu ambapo Waziri Mkuu amepokea fedha taslimu sh. milioni 25.62 pamoja na nguo zenye thamani ya sh. milioni mbili kutoka kwa wadau mbalimbali, Huku Shirika la Madini la STAMICO likichangia jumla ya shilingi milioni 20 katika fedha hizo.
Fedha hizo jumla ya shilingi milioni 20 zilizotolewa na STAMICO ni michango ya pamoja iliyotolewa na kampuni tanzu za KTCL, SAMIGOLD na STAMICO yenyewe.
Makabidhiano hayo yamefanyika katika hafla fupi iliyofanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es salaam leo.
(PICHA NA JOHN BUKUKU WA FULLSHANGWE-MAGOGONI DAR ES SALAAM)
1
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wao wa shilingi milioni 20 kwa Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa kulia kwake ni Mahende Michael Peter Mwanasheria Mkuu wa STAMIGOLD na waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Raymond Rwehumbiza Mratibu wa mradi Ununuzi wa Madini ya bati KTCL uliopo Kyerwa Mkoa wa Kagera, Alex Rutagwelela Kaimu Mkurugenzi wa Uchorongaji STAMICO , Beatrice Musa Lupi Mhasibu Mkuu STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
2
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akimuonyesha Waziri Mkuu Vocha ya malipo yaliyofanywa kwenye akaunti ya kuchangia wahanga wa Tetemeko la Ardhi Kagera kabla ya kukabidhi rasmi kwa waziri mkuu kutoka kushoto ni Mahende Michael Peter Mwanasheria na Mkuu wa Kitengo cha Sheria STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
3
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akikabidhi vocha hiyo kwa Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa kutoka kushoto ni Raymond Rwehumbiza Mratibu wa Ununuzi wa Madini ya KTCL Kyerwa Mkoa wa Kagera, Mahende Michael Peter Mwanasheria na Mkuu wa Kitengo cha Sheria STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
4
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akipiga picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO Bi. Zena Kongoi na ujumbe wake alioongozana nao kutoka shirika hilo.
5 7
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa aki akizungumza jambo na Bi. Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO mara baada ya makabidhiano hayo.
8
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Kassim Majaliwa na wageni mbalimbali waliofika ofisini kwake kutoa msaada kwa ajili ya wahanga wa Tetemeko la Ardhi mkoani Kagera wakimkubuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwa ni maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo chake miaka 17 iliyopita.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa