WATU WANNE WAFARIKI BAADA YA BASI LA SABUNI EXPRESS KUGONGAA USO KWA USO NA TOYOTA LAND CRUISER ENEO LA BUGORORA MKOANI KAGERA

 Watu wanne wanasadikiwa kufariki dunia baada ya Basi la Kampuni ya Sabuni Express linalofanya safari zake kati ya Karagwe na Mwanza kugongana uso kwa uso na Gari ndogo aina ya Toyota Land Cruiser iliyokuwa imebeba Masister eneo la Bugorora,ikitokea Bukoba mjini kuelekea Mutukura.
Baadhi ya miili ya marehemu waliofariki katika ajali hiyo

Askari wa Usalama barabarani akiwa eneo la tukio.

Endelea kutufuatilia kwa taarifa zaidi

UBUNGE VITI MAALUM VIJANA BUKOBA;ANTU MANDOZA AJITOSA KUCHUKUA FOMU

Mgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Bi. Antu Mandoza(Kulia) akirejesha Fomu ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana Bukoba katika ofisi za umoja huo Mjini Bukoba, ahaidi kuinua Vijana Kiuchumi endapo atapata nafasi ya kuwa Mbunge wa Vijana.(Habari Picha na Faustine Ruta/bukobasports).Mcheza kwao hutunzwa, Vijana wazidi kujitokeza kuwania nafasi mbalimbali za Uongozi. Binti Antu Mandoza mwenye kuonekana kuwa na umri miaka 22-25 Amerudisha Fomu za kuwania nafasi ya Ubunge Vijana Viti Maalumu kupitia CCM. Kwa Mahojiano mafupi ameongelea jinsi anavyopanga kuinua Maisha ya Vijana kwa kuwatengenezea Fursa na mbinu mbalimbali za kujiajiri pia kuwaonya kutokukubali kutumika vibaya na MAKUNDI ya Kisiasa tunapoelekea Uchaguzi kwani ni wajibu wetu Vijana kuilinda Amani yetu. Mgombea huyo pia amesema kuwa shauku yake kubwa ni kuwatumikia Vijana kwa kutatua changamoto ya Ajira na pia ametoa ahadi ya kushirikiana na Vijana bega kwa bega kuleta maendeleo katika Mkoa wa Kagera.
Binti Antu Mandoza akiweka sawa Kumbukumbu zake katika kitabu mbele ya karani Bi. Jasinta Benedicto wa Umoja wa Vijana Kagera.
Dada Antu Mandoza akiwa kwenye Ofisi za Umoja wa Vijana BukobaMgombea Ubunge Viti Maalum Vijana Bukoba Dada Antu Mandoza (kulia) akiptia Fomu yake ya Kuomba Ridhaa kuteuliwa kugombea Ubunge wa Viti maalum Vijana. Kushoto ni Bi. Jasinta Benedicto karani wa Umoja wa Vijana Kagera.
Mgombea Ubunge viti maalumu kupitia chama cha Mapinduzi dada Antu Mandoza akitoka katika ofisi za umoja wa vijana wa ccm Mkoa wa Kagera baada ya kuchukua fomu

BUKOBAWADAU MEDIA TUNAWATIA IDD NJEMA‏

 BUKOWADAU MEDIA , tunawatakia waislamu wote na wasomaji wetu popote duniani siku kuu ya njema yenye kheri na baraka.
Tunamuomba Mola wetu mlezi awarehemu wazee wetu wote waliotangulia mbele ya haki na awasamehe makosa yao.
“sifa zote njema ni za Mwenyezi Mungu ambaye ni vyake vyote vilivyomo Mbinguni na Ardhini. Na Akhera, sifa njema ni zake pia; Naye ni Mwenye Hekima na Mwenye Ujuzi wa kila jambo”.
Kwa utukufu wako huo tunakuomba Allah tuondolee madhila, maradhi na kila lililobaya kwetu waja wako wote, tutie imani ya kukutumikia wewe na utupe mwisho mwema hapa duniani na utufunike na rehma zako kesho akhera ili tuwe wenye kufuzu.
IDD MUBARAAK .
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa