Mganga Mkuu wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda
Na Lydia Lugakila - Bukoba
Wananchi katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wametakiwa
kutokutunza taka katika kaya zao na maeneo mbali mbali
ya biashara kwani kwa kufanya hivyo ni hatari kwa afya zao
huku watakaobainika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kauli hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Manispaa ya
Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda wakati
Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake
waliotaka kujua masuala mbali mbali yahusuyo afya
ndani ya Manispaa hiyo.
Mkenda amesema Manispaa hiyo imeweka utaratibu mzuri
wa ukusanyaji wa taka katika mitaa ambapo magari yanapaswa
kuzoa taka licha ya wananchi kutokutoa taka hizo kwa wakati.
0 comments:
Post a Comment