Mradi wa Umeme Vijijini (REA III) kufika Vijiji vyote nchini


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kwikuba kuhusiana na Mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akipokelewa na Mwenyekiti wa kijiji cha Kwikuba, Kamunyiro Kwibega.

Baadhi ya wananchi wakiagana na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) mara baada ya kumaliza kuzungumza nao
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (hayupo pichani).
Serikali imesema vijiji vyote ambavyo havikufikishiwa huduma ya nishati ya umeme vitapata huduma hiyo kupitia Mradi mkubwa wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III).

Hayo yamesemwa hivi karibuni na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo katika ziara yake katika kijiji cha Kwikuba, Mkoani Mara ya kukagua utekelezaji wa mradi wa Umeme Vijijini Awamu ya Pili (REA II) ambao unamalizika.

Katika maeneo mbalimbali aliyotembelea Waziri Muhongo alielezwa kuwa vijiji vya ndani havina umeme kwani umeme umeishia kwenye vijiji vilivyopo katika barabara kubwa na kwenye senta za biashara.

Waziri Muhongo alisema Serikali inatambua vijiji ambavyo havikufikishiwa huduma husika na hivyo aliwaasa wananchi katika vijiji hivyo kuwa na subira kwani lengo la Serikali ni kuhakikisha ndani ya miaka 10 vijiji vyote nchini view vimefikiwa na umeme.

Alisema Mradi huo wa REA III umetengewa zaidi ya trilioni moja ambayo ni mara tatu zaidi ya iliyotengwa kwa Mradi wa REA II ambao unamalizika kwa kuunganisha baadhi ya vijiji.

Aliongeza kuwa sasa hivi Serikali ipo katika utaratibu wa kuwapata Wakandarasi mahiri ambao watakabidhiwa jukumu la kutekeleza mradi huo ambao alisema ni mkubwa na wa kihistoria nchini.

Aidha akizungumzia mradi huo wa REA III, Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Mhandisi Amos Maganga alisema mbali na kuunganisha vijiji vyote, lakini pia mradi huo umelenga kuhakikisha unamaliza mapungufu yaliyojitokeza katika REA II.

Alisema katika utekelezaji wa mradi wa REA II kuna mapungufu yaliyojitokeza kwa sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwa na wigo mpana na hivyo kusababisha baadhi ya vijiji kurukwa na vingine kutofikiwa kabisa na vilevile uhaba wa baadhi ya vifaa katika maeneo mbalimbali.

Aliwaasa wananchi ambao vijiji vyao havijafikishiwa huduma ya nishati ya umeme kuwa na subira kwani mradi mkubwa wa Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (REA III) hautaacha kijiji.

KAIMU KATIBU MKUU UVCCM TAIFA SHAKA AFANYA ZIARA WILAYANI NGARA MKOA WA KAGERA NA KUZINDUA MIRADI MBALIMBALI YA UMOJA HUO

  Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC)akizungumza na
Wajumbe wa Baraza la UVCCM pamoja na Wajumbe wa Sekretariet ya CCM Wilayani
Ngara Katika  Kikao Cha Ndani Kilicho Fanyika katika Ukumbi wa Engubenako
Wilayani Ngara.
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akiwasili katika
Kijiji Cha BENACO Wilayani Ngara, Shaka yupo  kwa ziara ya kuimarisha uhai
wa chama, kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya
CCM 2015_2020
 Mwenyekiti wa uvccm Mkoa wa Kagera Bw. Yahya Kateme akizungumza
kumkaribisha Ndg: Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka
Kuzungumza na Wajumbe wa Baraza la UVCCM pamoja na Wajumbe wa Sekretariet
ya CCM Wilayani Ngara
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC)akizungumza na
Wajumbe wa Baraza la UVCCM pamoja na Wajumbe wa Sekretariet ya CCM Wilayani
Ngara Katika  Kikao Cha Ndani Kilicho Fanyika katika Ukumbi wa Engubenako
Wilayani Ngara
 :Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akizindua Mradi wa
kikundi cha Vijana wajasiliamali cha Ufugaji wa Nyuki na Shamba la Upandaji
wa Miti katika kijiji cha Nyaruku Wilayani Ngara.
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akikagua Mradi
wa Usambazaji wa Umeme Vijijini katika kijiji cha Nyankenda ikiwa ni
Utekelezaji wa Ilani ya CCM 2015_2020
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akikagua
Ukamilishaji wa Agizo la  Utengenezaji wa Madawati  katika Shule ya Msingi
Rulenge Jinsi lilivyo Kamilika kama alivyotoa agizo Mhe:Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli
 Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) akimkabidhi
mmoja kati ya Wazee 25 waliopokea Vyeti Vya Matibabu ya bure kwa wazee
katika kijiji cha kijiji cha Mumiramila Wilayani Ngara.
 Mwandishi wa Gazeti la Uhuru Bw.Antari Sangali pamoja na wazee wakijiji
cha Mumilamila Wilayani Ngara wakimsikiliza kwa makini Kaimu Katibu Mkuu
UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC)alipo kua akigawa Vyeti kwaajili ya
Matibabu ya Bure kwa wazee.
:Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Taifa Shaka Hamdu Shaka (MNEC) alipo zindua
Mradi wa Shamba la Uvccm wilayani Ngara kwa ajili ya Shughuli Mbali mbali
za kilimo kwa Vijana Wilayani humo ikiwa ni Utekelezaji wa agizo lake
alilotoa kwa Makatibu wote kuandaa miradi Mbali mbali ili kukwamua Vijana
kiuchumi kama kauli Mbiu yake isemayo'' SIASA NA UCHUMI''(picha na woinde Shizza.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa