*TAMKO - STATEMENT YA ASKOFU METHOD KILAINI DHIDI YA GAZETI LA MWANANCHI LEO 16 NOV





Askofu Method Kilaini

TAMKO – STATEMENT

Kwa masikitiko makubwa nimesoma katika gazeti la Mwananchi kwamba nimeiponda safu ya uongozi na sekretariati ya CCM. Mimi sijaongea na gazeti lolote juu ya uongozi wa CCM na wala sina nia au sababu ya kuuponda uongozi huo. Ni vibaya kwa gazeti lo lote lile kutumia jina la mtu kwa kueneza maoni yake. Kama ni waugwana natumaini watasahihisha waliyoyaandika. Nasikitika sana kwa walikwazwa na hilo. Askofu Kilaini

Askofu Method Kilaini
Bukoba Catholic Diocese


Boti yazama,saba wafa

Watu saba wamefariki dunia baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama katika Ziwa Victoria eneo la hifadhi ya kisiwa cha Rubondo Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Ajali hiyo ilitokea Novemba 10, mwaka huu majira ya usiku wakati watu hao wakiwa katika shughuli za uvuvi jirani na eneo la hifadhi ya kisiwa cha Rubondo.

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu, Diwani wa Kata ya Ikuza, Fortunatus Wazia, alisema kuwa watu hao walikuwa ni wavuvi kutoka sehemu mbalimbali za ndani na nje ya Wilaya ya Muleba.

Wazia alifafanua kuwa wavuvi hao walikumbwa na mkasa huo baada ya chombo walichokuwa wakisafiria kuzama.

Kwa mujibu wa diwani huyo, wavuvi hao walikwenda kuvua samaki kwenye kisiwa cha Rubondo kinyume cha sheria kwa kuwa ni eneo la hifadhi na boti hiyo ilizama kutokana na kutokuwa na ubora.

Alifafanua kuwa kutokana na hali hiyo, ilianza kuvuja maji wakati wakirejea kisiwani Ikuza kabla ya kuzama.

Kwa mujibu wa Wazia, watu hao waliondoka katika kisiwa cha Ikuza kwenda kwenye hifadhi ya Rubondo Novemba 8, mwaka huu na walipita njia za panya wakikwepa walinzi wa hifadhi wasiwakamate kwa kuwa walikuwa wanafanya ujangili.

Diwani huyo aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Baruya Masala, mkazi wa Muganza wilayani Chato; Alex Mwita, mkazi wa Tarime; Kipara Kasukari, mkazi wa Kata ya Mushabago wilayani Muleba na mwingine amejulikana kwa jina moja la Niko, mkazi wa Sengerema.

Wengine ni Obadia Yohana, mkazi wa Muganza; Juma Kengere, mkazi wa Itale Chato; na mwinge aliyetambuliwa kwa jina moja la Robert, mwenyeji wa Wilaya ya Biharamulo.

Wazia alisema kuwa baadhi ya miili ya marehemu hao ilitambuliwa na ndugu na jamaa zao na tayari ilimeshachukuliwa kwa ajili ya mazishi.

Hata hivyo, alisema maiti watatu hawakutambuliwa na ndugu mapema na kulazimika kuzikwa katika eneo la ufukweni mwa Ziwa Victoria katika kisiwa cha Ikuza wilayani Muleba.

Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Philip Kalangi, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na wavuvi hao kufariki dunia.

Kamanda Kalangi aliongeza kuwa Jeshi la Polisi mkoani Kagera linaendelea kuchunguza kwa lengo la kubaini chanzo cha ajali hiyo.

WADAU WA ELIMU CHATO WALALAMIKIA ELIMU YA AWALI



Watoto wa awali wa shule ya msingi Kalema.
 Watoto wa awali wa shue ya msingi Chato.
-
Na Daniel Limbe,Chato

LICHA ya serikali kuhamasisha
uanzishwaji wa elimu ya awali katika shule zote za msingi hapa nchini
kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kimaarifa watoto
ambao hawajafikia umri wa kuanza elimu ya msingi,hatua hiyo imeonekana
kulalamikiwa sana na baadhi ya wadau wa elimu katika wilaya ya chato
mkoani geita kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu mbalimbali ya
kufundishia.

Wakizungumza na mwandishi wa habari
hizi baadhi ya walimu wakuu wa shule za msingi Kalema,Kitela na Chato
wamesema upatikanaji wa elimu ya awali kwa
watoto ni changamoto kubwa kwa serikali kutokana na ukosefu mkubwa wa
vitabu vya kufundishia,vifaa vya kujifunzia na uhaba wa walimu.

Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule ya
msingi Chato Mwita Chacha shule yake inawanafunzi wa awali 300 na
kwamba watoto hao wanamwalimu mmoja na kwamba
hakuna madawati ya kukalia wala vifaa vya kujifunzia kwa vitendo hali
inayosababisha watoto wengi kushindwa kupata elimu iliyokusudiwa.

Amesema kitendo cha mwalimu mmoja
kufundisha watoto 300 hakiendani na mpango wa kitaifa wa utoaji elimu
ambao unamtaka mwalimu mmoja kufundisha watoto
40 huku akiiomba serikali kuimalisha miundombinu ya kufundishia
itakayosaidia kuboresha elimu kwa watoto wa shule za awali.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule
ya msingi Kalema Tano Bara amesema ili elimu ya awali iweze kupatikana
kwa ufanisi kuna haja kubwa kwa serikali
kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kununua vitendea kazi vya
kufundishia na kufundishiwa hatua itakayorahisisha upatikanaji wa elimu
bora kwa watoto wa awali ikilinganishwa na hali ilivyo hivi sasa.

Aidha uchunguzi wa Mwandishi wa habari
hizi umebaini aslimia 95 ya shule za awali wilayani chato hakuna vitabu
vya kufundishia watoto badala yake
walimu wa madarasa hayo hulazimika kutumia mihutasari inayotoa miongozo
ya kutolea elimu hiyo huku madawati na vifaa vingine vya kujifunzia
vikionekana kitendawili.

Kutokana na hali hiyo baadhi ya watoto
wa awali imeonekana ni vigumu kwao kujifunza kwa ufasaha kutokana na
baadhi yao kukaa chini na wengine kukalia
mawe wakati wa kujifunza hivyo kusabisha watoto kuwa na miandiko
isiyofaa.

Alipotakiwa kujibu malalamiko hayo
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chato Shaban Ntarambe alidai kuwa
yeye siyo msemaji licha ya kudai kuwa
serikali inayafahamu mapungufu yaliyopo na kwamba taratibu bado
zinafanyika ili kutatua hali hiyo.

Aidha amedai kuwa mwongozo alionao
unamuelekeza kusimamia uandikishwaji wa watoto wa shule za awali kila
kijiji na kwamba hatua zingine zitafuatwa
kulingana na mpango wa serikali.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa