KAMATI YA BUNGE YATEMBELEA MAPORI YA AKIBA YA BIHARAMULO, BURIGI, KIMISI (BBK) MKOANI KAGERA


Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Nape Nnauye akiwaongoza baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo kushuhudia maporomoko ya maji ya Rusumo yaliyopo wilayani Ngara ambapo moja ya vyanzo vyake vikubwa vya maji vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa Kagera.
Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakipewa maelezo kuhusu mipaka ya Pori la Akiba ya Biharamulo kutoka ziwa Victoria katika kituo cha Katete kutoka kwa Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) wakati Kamati hiyo ilipotembelea mapori yaliyopo mkoani Kagera mwishoni mwa wiki
Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) akiwaonesha Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii katika ramani mahali ambako Pori la Akiba la Burigi lilipoanzia wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), yaliyopo mkoani Kagera hayo mwishoni mwa wiki mkoani Kagera
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Nape Nnauye akiwazungumza na baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo mara baada ya kujionea Pori la Akiba la Burigi katika wilaya ya Karagwe ambayo ni moja ya kati avyanzo vyake vikubwa vya maji ambavyo vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa Kagera.Wajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakiangalia hema ambalo askari wanyamapori hulitumia kumpumzika wakiwa katika Mapori wakati wanapofanya doria za kuwabaini majangili.Meneja wa mpaka katika Tanzania na Rwanda ambaye pia ni Afisa Mwandamizi wa Forodha, Polycarp Lashau akiwaongoza Wajumbe wa kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kushuhudia maporomoko ya maji ya Rusumo yaliyopo wilayani Ngara ambapo moja ya vyanzo vyake vikubwa vya maji vimeanzia katika Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) wakati Kamati hiyo ilipofanya ziara mwishoni mwa wiki mkoani wa KageraWajumbe wa Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii wakipewa maelezo kuhusiana na mali mbalimbali za watuhumiwa wa ujangili zikiwemo baiskeli na pikipiki zilizokamatwa katika kituo cha Katete kwenye Pori la Akiba ya Biharamulo kutoka kwa Meneja wa Mapori ya Biharamulo, Burigi, Kimisi (BBK), Bw. Bigilamungu Kagoma (wa kwanza kushoto) wakati Kamati hiyo ilipotembelea mapori yaliyopo mkoani Kagera hayo mwishoni mwa wiki
(PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT)

Kamati ya Ardhi, Maliasili na Utalii ambayo ipo mkoani Kagera imeridhishwa na utendaji kazi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) baada ya kutembelea Mapori ya Akiba ya Biharamulo, Burigi na Kimisi (BBK) kuangalia kazi za uhifadhi zinazofanywa ambapo wameipongeza TAWA kwa kitendo cha kurudisha hali ya mapori hayo ikiwemo kurejea kwa wanyamapori na uoto wa asili ambapo awali mapori hayo yalikuwa yameharibiwa kwa kasi kutokana na makundi ya mifugo kufanya malisho katika maeneo hayo.

Katika ziara hiyo,iliyoanzia katika Wilaya ya Biharamulo, Wajumbe wa Kamati hiyo waliweza kushuhudia eneo la Pori hilo lilipoanzia katika ziwa Victoria na baadaye kushuhudia Pori la Burigi lililopo katika wilaya za Karagwe na Biharamulo na badaye Pori la Kimisi ambalo lipo katika wilaya mbili za Karagwe na Ngara.

Hata hivyo,Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Nape Nnauye aliridhishwa na masuala ya uendeshaji wa mapori hayo huku akiahidi kuyasaidia mapori hayo kwa kuishauri serikali iweze kuwekeza miundombinu ili kukuza utalii katika ukanda wa ziwa Victoria

‘’Tunatambua kuwa TAWA ni changa haijaanzishwa muda mrefu lakini ndani ya kipindi kifupi imeweza kufanya mambo mazuri katika kulinda Maliasili zetu , Sisi kamati tumeridhisha na utendaji wake’’ alisema Mwenyekiti

Kutokana na utendaji kazi wa Mamlaka hiyo , ‘Mwenyekiti wa Kamati hiyo iliahidi kuwa watalishauri na pamoja na kuishawishi Serikali iweze kuongeza pesa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019 ili iweze kutimiza wajibu yake.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla aliielezea kamati hiyo kuwa TAWA ipo mbioni kubadili mfumo wake katika mapori hayo ambapo badala ya kuendelea kufanya shughuli za uwindaji wa kitalii pekee wamepanga kuanzisha utalii wa picha ili kufungua fursa za kiuchumi katika ukanda huo.

Aidha, Waziri Kigwangalla alisema kuwa kutokana na Mapori hayo kurejea katika uasilia wake baada kuharibiwa kwa kiasi kikubwa na uvamizi wa mifugo hali iliyopelekea hadi wanyamapori kuhama, Wizara inafanya utafiti ili kuongeza baadhi ya wanyama katika Mapori hayo ili kuweza kuwavutia watalii zaidi kutembelea maeneo hayo.

Aliongeza kuwa, mapori hayo yana sifa ya pekee za kumvutia mtalii yeyote aweze kutembelea katika maeneo hayo huku ukitaja wanyamapori wanne wakubwa kuwa wanapatika katika mapori hayo isipokuwa faru pekee.

Awali kamati hiyo ilipokea taarifa kutoka kwa Wenyeviti wa Kamati za ulinzi na usalama za wilaya ambapo miongoni mwa mambo yaliyojitokeza uvamizi wa maeneo ya mapori ya akiba kwa kuanzisha shughuli za kilimo pamoja na kulisha mifugo ndani ya hifadhi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa TAWA, James Wakibara alisema moja ya mikakati ya TAWA ni kubadilisha aina ya biashara kwa kuanza kuchanganya ambapo TAWA itaendesha biashara ya uwindaji wa vitalu pamoja na utalii wa picha katika mapori hayo kwa lengo la kuiongezea serikali mapato

Alisema Serikali ipo katika mchakato wa kuboresha miundombinu kwa kuanza na barabara ndani ya mapori hayo ili kuweza kuwavutia wawekezaji kujenga hoteli mbalimbali ambazo watalii watazitumia kwa ajili ya kupumzika.

MKUU WA MKOA KAGERA AAGIZA MKANDARASI KUKAMATWA NA KUFIKISHWA OFISINI KWAKE AKIWA NA PINGU MIKONONI BAADA YA KUITIA SERIKALI HASARA

 Baadhi ua Wabunge wa Mkoa wa Kagera Wakifuatilia Mada Katika kikao
 Baadhi ya Waandishi wa Habari Wakitekeleza Majukumu yao Katika Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoani Kagera  
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu Katikati Akiongea na Wajumbe wa Kikao cha Bodi ya Barabara Mkoani Kagera Hawapo Pichani
Wajumbe Wakifuatilia Mada katika Kikao cha Bodi ya barabara Mkoani Kagera
Na Sylvester Raphael
Mkuu wa Mkoa wa Kagera aagiza  Mkandarasi wa Kampuni ya MECCO aliyeshinda zabuni  ya ujenzi wa barabara zenye thamani ya shilingi bilioni saba na kukataa kusaini mkataba wa  kuanza ujenzi katika Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba kukamatwa  na kufikishwa  Ofisini kwake akiwa na pingu mikononi ili kutoa sababu za kuitia Serikali hasara.
Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu alitoa agizo hilo kwa Kamanda wa Polisi Mkoa kwenye kikao cha Bodi ya Barabara kilichofanyika Mkoani Kagera Machi 8, 2018 ambapo katika kuwasilisha hoja Mstahiki Meya wa Manispaa ya Bukoba Chief Karumuna  kumuomba Mkuu Mkoa kumchukulia hatua Mkandarasi huyo baada ya kugoma kusaini mkataba wakati alishinda zabuni ya ujenzi wa barabara hizo.
Chief Karumuna alisema kuwa Manispaa ya Bukoba imepata hasara baada ya Mkandarasi kukataa kusaini mkataba wa kuanza ujenzi wa barabara zenye thamani ya shilingi bilioni saba na zabuni kutangazwa tena upya, pia alisistiza kuwa fedha hizo zilitolewa na Benki ya Dunia na utekelezaji wa miradi yake ni wa kipindi maalumu kwa hiyo Mkandarasi huyo amechelewesha muda wa utekelezaji.
Katika kikao hicho ambacho Mkuu wa Mkoa ni Mwenyekiti aliwasistiza Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini TARURA Mkoa wa Kagera kuhakikisha wanatengeneza barabara za mipakani ili kuimarsha ulinzi na usalaama wa mkoa na na chi kwa ujmla. Barabara hizo ni Bubale-Missenyi Runch- Kakunyu  Kilomita 32.5, Bubale – Kamwema Kilomita 17.8  Wilayani missenyi na barabara ya Nyabishenge-Nyakanoni-Ibanda Game Reserve kilomita 15 Wilayani Kyerwa.
Vilevile Meneja wa Wakala wa Umeme na Ufundi (TEMESA) Mkoa wa Kagera ameagizwa na kikao hicho kusitisha mara moja tozo ya shilingi 80,000/= ya ukaguzi wa magari ya Serikali pale yanapotakiwa kukaguliwa ili yakatengenezwe baada ya wajumbe kuwasilisha sheria kikaoni inayoelekeza kuwa magari ya Serikali yanatakiwa kukaguliwa bure. Hadi Mkuu wa mkoa atakapopata walaka unaoruhusu kutoza magari ya Serikali.
Mkoa wa Kagera unahudumia barabara zenye mtandao wenye jumla ya kilomita 7,505.42 kati ya hizo, kilometa 675.46 ni barabara za lami, kilometa 2,791.56 barabara za changarawe na kilometa 4,038.96 zikiwa in barabara za udongo.
Mkoa wa Kagera kwa mwaka wa fedha 2017/18 uliidhinishiwa shilingi Bilioni 10,710.05 kwajili ya matengenezo ya kazi za barabara na ujenzi wa madaraja. Pia mkoa umeidhinishiwa shilingi bilioni 14,180.937 kwa ajili ya matengenezo ya Barabara Kuu na Barabara za Mkoa kwa mwaka wa fedha 2017/18
Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Mkoani Kagera Mkuu wa Mkoa wa Kagera amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Karagwe Godfrey Mheluka kumkamata na kumpeleka ofisini kwake kijana anayemtesa mama yake mzazi kwa kutaka kumnyanganya shamba lake na mama huyo ameshinda kijana huyo mara mbili Mahakamani.
“Mtafute kijana huyo na kumleta kwangu nijue ana matatizo gani ili tumsaidie maana atamuua mama yake, hana uchungu na mama yake mzazi. Mama huyoaliwasilisha kilio chake katika mkutano wa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi Mhe. Lukuvi Wilayani Karagwe lakini kijana huyo bado anaendelea kumsumbua mama yake mzazi.” Alifafanua Mkuu wa Mkoa Kijuu.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa