WANAOTUNZA TAKA NDANI YA SAA 48 KATIKA KAYA ZAO MANISPAA YA BUKOBA WAONYWA
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda
Mganga Mkuu wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda
Na Lydia Lugakila - Bukoba
Wananchi katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera wametakiwa
kutokutunza taka katika kaya zao na maeneo mbali mbali
ya biashara kwani kwa kufanya hivyo ni hatari kwa afya zao
huku watakaobainika kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kauli hiyo imetolewa na Mganga Mkuu wa Manispaa ya
Bukoba Mkoani Kagera Dkt. Peter Mkenda wakati
Akizungumza na Waandishi wa habari ofisini kwake
waliotaka kujua masuala mbali mbali yahusuyo afya
ndani ya Manispaa hiyo.
Mkenda amesema Manispaa hiyo imeweka utaratibu mzuri
wa ukusanyaji wa taka katika mitaa ambapo magari yanapaswa
kuzoa taka licha ya wananchi kutokutoa taka hizo kwa wakati.
MWL. MBELWA AIKACHA CHADEMA, APOKELEWA NA MAKAMU MWENYEKITI WA CCM TAIFA WASIRA
Na Grace Mpondwe,Kagera
Katika hali isiyotarajiwa leo Machi 25, 2025 aliyekuwa mgombea wa kiti cha ubunge jimbo la Biharamulo mwaka 2020 kupitia CHADEMA amekihama chama hicho na kujiunga na CCM akipokelewa na kukabidhi kadi kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Masato Wasira akiwa mkoani Kagera.
Ziara hiyo ni ya kwanza kwa kiongozi huyo mkubwa wa CCM kuifanya mkoani Kagera tangu aidhinishwe na chama hicho kushika wadhifa huo mnamo 18-19 Januari, 2025.
Mwanasiasa huyo kijana amesema kuwa CCM ni chama kilichokamilika kimfumo kwa ajili ya kuiongoza nchi kuleta maendeleo huku amani ikiwa ni kipaumbele cha kudumu. Mwalimu amesema kuwa chama chake cha awali CHADEMA bado kinajisuka huku kikiteswa na zimwi la uchanga, upendeleo, utovu wa nidhamu na mikakati isiyofanya kazi.
Mwalimu alisema "CHADEMA leo wanahubiri NO HATE, NO FEAR!, kesho wanahubiri JOIN THE CHAIN!, keshokutwa wanahubiri STRONGER TOGETHER!, mtondogoo wana NO REFORM, NO ELECTION, Bangi za LEMA zikikolea kichwani anawaimbisha tena wanachama TONE TONE, mara NIMO", hakuna mkakati unaokamilika na kuleta matokeo kwa chama. Waswahili husema miruzi mingi hupoteza mbwa. Nimeamua kukihama chama hicho kwa hizo inconsistencies katika mikakati yake"
Kuhusu suala NO REFORM NO ELECTION, Mbelwa amesema CHADEMA imeibuka na mkakati huo kutokana na maandalizi hafifu ya kushiriki uchaguzi hivyo hiyo kauli inatumiwa kama kichaka cha kujifichia ili wasishiriki uchaguzi".
Mbelwa aliongeza kwa kusema kuwa "kitendo kinachopangwa na CHADEMA cha kuzuia uchaguzi usifayike ni ndoto ya mchana kwa sura moja na ni uhaini kwa sura nyingine. Mimi siwezi kuoteshwa ndoto hizo na kamwe siwezi kuendelea kufikiria kufanya uhaini wa namna hiyo kwa nchi yangu, sikuwahi kuwa mwanasiasa mwenye malengo machafu kwa nchi yangu".
Mwl. Mbelwa amesema "ni vigumu kwa chama kilichoshindwa kuweka utulivu kwenye ofisi moja ya makao makuu iliyopo Mikocheni kuleta utulivu kwenye nchi yenye kilomita za mraba 945,000 na watu wake milioni 60".
Ameongeza kuwa kutokana na mahaba waliyonayo Watanzania kwa CCM, ukipingana na CCM unajitakia taabu za maksudi pamoja na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwemo moyo kuvimba.
Amesema "Mimi Mbelwa Petro nimeona nitosheke na taabu nilizozipata kwa kuwa mwanaCHADEMA, sasa inatosha."
"Mwaka 2020 nilipogombea ubunge jimbo la Biharamulo, nilipata shida za kujitakia na baada ya uchaguzi kuisha niliambulia kuitwa Mbunge wa wananchi, nikamuuliza Mh. Mbowe, sisi wabunge wa wananchi tutakwenda kuapia wapi? Akasema, atanijibu baadae. Hajanijibu mpaka leo tarehe 25 Machi, 2025.
"Nikamuacha nikaenda kwa Kaka Lissu kwa kuwa yeye ni mwanasheria, nikamuuliza vipi Mzee sisi wabunge wa wananchi tunaapa kwa katiba ipi? Ni lini? Na wapi?".
Lissu akaniambia niwe mtulivu kwani naye yupo anatorokea Ubelgiji kutokana na hali kuwa ngumu. Nilichoka, na kupata taabu mara mbili". Ameongeza.
Mbelwa amesema "nisiseme mengi, kwa sasa nawaomba wanaCCM mnipokee, kuanzia sasa nimeacha kukunjishwa ngumi pasipo kuwa na mtu wa kupigana naye".
Kuhama kwa kada huyo linaweza kuwa pigo kwa CHADEMA jimbo la Biharamulo kwa kuwa mwanasiasa huyo alikuwa na ushawishi mkubwa hasa kwa vijana katika jimbo na mkoa mzima kwa ujumla.
KAGERA, GEITA KUANZA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AGOSTI 5,2024
Meza kuu ikiongozwa na Makamu Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk (katikati) Mjumbe wa Tume, Mhe. Magdalena Rwebangira (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Elimu ya Mpiga Kura, Bi.
Giveness Aswile
Viongozi wa kimila ni miongoni mwa wadau muhimu wa Uchaguzi hivyo Tume iliwashirikisha viongozi hao kutoka Kagera.
Wadau kutoka makundi mbalimbali ya wanawake na vijana nao walishiriki.
Makamu Mwenyekiti Wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Mhe. Mbarouk Salim Mbarouk akiongoza majadiliano wakati wa Mkutano huo.

Viongozi wa kimila ni miongoni mwa wadau muhimu wa Uchaguzi hivyo Tume iliwashirikisha viongozi hao kutoka Kagera.
Wadau kutoka makundi mbalimbali ya wanawake na vijana nao walishiriki.
Wahariri kutoka Vyomb0 vya habari nao walishiriki.
Vyama vya siasa nao walishiriki
Viongozi wa Dini nao walishiriki






