Kampuni ya Tigo yatoa Misaada kituo cha kulelea Watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba‏


Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akikabidhi misaada mbalimbali Mwenyekiti wa kamati ya shule ya kulelea watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba Bi. Evelyne Mwijage juzi. Kampuni ya Tigo ilitoa misaada kwenye kituo hicho
Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akikabidhi misaada mbalimbali Mwenyekiti wa kamati ya shule ya kulelea watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba Bi. Evelyne Mwijage juzi. Kampuni ya Tigo ilitoa misaada kwenye kituo hicho



Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akiongea na wanahabari,viongozi  na watoto wa kituo cha kulelea watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba.

Meneja wa Mauzo Mkoa wa Kagera, Sadoki Phares akiongea na wanahabari, viongozi na  watoto wa kituo cha kulelea watoto Yatima cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba.

Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Tigo Kanda ya Ziwa, Beatrice Kinabo(kushoto) na Meneja wa Duka la Tigo Bukuba, Lilian Mwise (aliyebeba mtoto).


Watoto wa Kituo cha kulelea watoto cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba wakifuatilia kwa makini.

Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Ziwa, Ali Maswanya akitembea na watoto wa kituo cha Mugeza mara baada ya kukabidhi misaada.A

Watoto wa Kituo cha kulelea watoto cha Mugeza Mseto Manispaa ya Bukoba wakifuatilia kwa makini.

HARAKATI ENDELEVU ZA KIKUNDI CHA “BUKOBA MPYA PROJECT” ZOEZI LA KUTOKOMEZA MAZALIA YA MBU KATA ZA MANISPAA YA MJI BUKOBA‏


HARAKATI ENDELEVU ZA KIKUNDI CHA “BUKOBA MPYA PROJECT”

ZOEZI LA KUTOKOMEZA MAZALIA YA MBU KATA ZA MANISPAA YA MJI BUKOBA

Ndugu Wadau,

“Bukoba Mpya Project” ni zao la harakati endelevu chini ya Bukoba Wadau Media katika kuchangia kuhamasisha Wanabukoba wa ndani na nje ya Tanzania kushiriki katika kuinua hali ya mji na maisha ya wakazi wa Bukoba.  Wanachama wa harakati hizi ni waamini wa itikadi ya UMOJA na MAENDELEO. Mpaka sasa jumla ya wanachama wasioupungua 50 kutoka ndani na nje ya Bukoba na Tanzania kwa ujumla wanashiriki harakati hizi.

Wakiongozwa na imani kwamba “maendeleo yanaletwa na mimi”, Wana Bukoba Mpya wamepanga kuanza jitihada ya kupambana na Malaria kwa kutokomeza mazalia ya mbu kwenye maeneo yote ya Manispaa ya Bukoba. Jitihada hii itatekelezwa kwa zoezi la kupulizia dawa za kuua mazalia ya mbu kwenye Kata zote 14 za Manispaa ya Bukoba. Zoezi litaanzia na Kata za Greenbelt  (Kahororo,Buhembe, Kitendaguro ,Ijuganyundo,Nyanga,Kibeta na Nshambya) mara tu baada ya siku kuu kuisha kisha litaendelea kwenye kata zingine zote kadri ratiba itakavyotolewa.

Kila mmoja anayeguswa na athari za mbu na anavutiwa na jitihada hii anaalikwa kushiriki kwa njia moja au nyingine. Unaweza kufanya hivyo kwa:

·         Kuthibitisha kushiriki moja kwa moja kwenye zoezi tarehe na mahali litakapofanyika
·         Kwa kuhamasisha ndugu na jamaa zako wafike kushiriki (hii ni kwa walio mbali na nje ya Tanzania)
·         Kwa kuchangia pesa, madawa na vifaa vya zoezi (orodha ya vifaa na utaratibu utapatiwa)

Viongozi, Watendaji na Wananchi kwa ujumla waombwa kutoa ushirikiano na kushiriki kwa kadri wanavyoweza pale zoezi hili litakapofanyika katika maeneo yao.

Kwa mawasiliano na maelezo zaidi juu ya jinsi ya kushiriki wasiliana nasi kwa njia zifuatazo:
Mob: 0784 505045 / 0768 397241 /0713 883020 /0754 505043.


Imetolewa na:
Kitengo cha Uhamasishaji Jamii
Bukoba Wadau Media


 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa