TMA yatahadharisha wananchi kuhusu ongezeko la joto, Mvua kubwa isiyotabirika yaja, TMA yatahadharisha wananchi

Dar es Salaam. Mvua kubwa isiyotabirika inatarajiwa kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini hasa katika ukanda wa Pwani ya Kaskazini, maeneo ya Dar es Salaam, Tanga, Unguja na Pemba; pia katika ukanda wa Kaskazini Mashariki kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha na Manyara.
Akitoa taarifa ya hali ya hewa jana kwa Januari na Februari mwaka ujao, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Dk Agness Kijazi alisema mvua ya msimu katika maeneo hayo inatarajiwa kwisha leo.
Hata hivyo, alisema mvua kubwa ya nje ya msimu inatarajiwa katika kipindi cha Januari, 2015. Dk Kijazi alisema hali kama hiyo pia itaikumba mikoa ya Kagera, Mwanza, Shinyanga na Geita.
“Maeneo mengine yanayopata msimu mmoja wa mvua kwa mwaka yatakuwa na mvua ya wastani. Maeneo hayo ni Mbeya, Rukwa, Katavi, Iringa, Lindi, Dodoma na Mtwara.
Dk Kijazi alisema mvua hiyo inasababishwa na ongezeko la joto linalolifanya anga kushindwa kutengeneza unyevunyevu ambao hugeuka kuwa mvua. “Ninawashauri wananchi kuchukua hatua ya kujikinga na athari za kiafya na mazingira zinazoweza kusababishwa na ongezeko la joto linaloendelea sambamba na mvua kubwa inayonyesha,” alisema Dk Kijazi.
Juzi, mvua kubwa ilinyesha jijini Dar es Salaam kwa saa mbili na kusababisha vifo vya watu wawili katika Wilaya ya Kinondoni kuleta kero kwa wasafiri wanaotumia vyombo vya moto na watembea kwa miguu.
Mitaa ya Azikiwe, Bibi Titi na Morogoro ambayo juzi ilijaa maji, jana ilionekana kuwa mikavu baada ya maji yote kukauka.
huku watumiaji wa barabara wakiendelea na shughuli zao kama kawaida.
Yusuph Said, mmoja wa wafanyabiashara wa magezeti Mtaa wa Azikiwe, alisema eneo hilo hujaa maji kila mvua inaponyesha na kuwasababishi kufanya kazi yao katika mazingira magumu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura aliliambia gazeti hili jana kuwa hakuna madhara zaidi yaliyotokea ukiacha matukio ya watu wawili kufariki dunia kutokana na mvua hiyo.
Naye Kamanda wa Polisi Ilala, Mary Nzuki alisema: “Mkoani kwangu sijapokea taarifa yoyote ya maafa yaliyosababishwa na mvua mpaka sasa.” Kamanda Kihenya Kihenya wa Mkoa wa Kipolisi Temeke naye alisema hajapokea taarifa yoyote ya maafa.

Akizungumzia matukio ya mvua kipindi cha Oktoba – Disemba, 2014, Dk Kijazi alisema maeneo mengi ya nchi yalipata mvua za wastani hadi juu ya wastani isipokuwa maeneo machache ya mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Dodoma (Hombolo), Kilimanjaro (Same), Njombe, Mtwara na Lindi ambayo yalipata mvua za chini ya wastani.
Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa matukio ya mvua hizo ambayo yaliambatana na vipindi vifupi vya upepo mkali, yalisababishwa na kuimarika kwa ukandawa mvua magharibi mwa nchi ambao uliambatana na kuwepo kwa makutano ya upepo.
“Wananchi wajenge pia utamaduni wa kupanda miti ili kusaidia kupunguza kasi ya upepo unaombatana na mvua kubwa ambazo zinaweza kusababisha uharibifu wa mali na madhara kwao,” alisisitiza Dk Kijazi.
Peter Elias, Bakari kiango na Hadija Salum wa Mwananchi

BUNGE "RUBBER STAMPED" IPTL PROPOSAL



THE resolution passed by the National Assembly to nationalise the Independent Power Tanzania Limited (IPTL) was a rubber stamp of a proposal earlier given by Standard Chartered Bank (Hong Kong) Limited, it has been learnt.

It had been revealed that Standard Chartered Bank wrote to the then Chief Executive Officer of the Tanzania Electric Supply Company Limited (Tanesco), Dr Idris Rashid, proposing the nationalisation of IPTL so that it could be paid a sum of 112 million US dollars.

The letter, dated September 22, 2009, shows that the bank proposed to Tanesco’s legal advisers that the government of Tanzania immediately considers nationalisation of IPTL and that move would be with the support of the bank and with the express objective of implementing the agreed plan.

“If nationalisation was to be agreed upon and implemented, then the whole process could be conducted through the Tanzanian Parliament.

There would be no need to involve courts,” reads a section of the letter in question. The bank alleged in the letter that it believed it has been treated unfairly and inequitably before Tanzanian courts and therefore, was firmly of the view that any attempt to implement its agreed plan through the office of the provisional liquidator of IPTL at the time, would suffer the same fate.

It wrote further that rather than seeking to resolve its claims through international litigation and in light of the progress made with Tanesco on the agreed plan, the bank was prepared to give an opportunity for an early settlement through a consensual nationalisation.

“Accordingly, the bank and its lawyers would, if asked, work with you (Dr Rashid) and your legal advisers in an effort to secure the approval of the committee to a nationalisation proposal, within the next 14 days,” the letter further explains.

The bank went on to propose that the matter could be passed from there to the Cabinet for it to deliberate and with the approbation of the Cabinet, a bill could be placed before Parliament within a timetable consonant with Tanesco’s desire to dispatch power from the project.

“If Tanesco and government of Tanzania manifest a real desire to see a nationalisation achieved quickly and absent any avoidable delay, it can count on full support of the Bank, which would not in such circumstances, see any need to take matters further in any international forum,” the Bank’s letter says.
On November 29, this year, while deliberating the Escrow Account Saga, the National Assembly passed eight resolutions, including a proposal to the government to nationalise the IPTL power plant so that it becomes state owned company through Tanesco.

Addressing the nation through elders from Dar es Salaam Region, President Jakaya Kikwete ruled out the possibility to nationalise the power plant, saying such attempt would jeopardise the government’s good intention of encouraging foreign investment in the country.

SOMA HOJA ZA WAZIRI TIBAIJUKA KWANINI HATAKI KUJIUZULU JUU YA SAKATA LA ESCROW

  HOJA ZA MSINGI ZA PROFESA ANNA KAJUMULO TIBAIJUKA KWA NINI HAONI MANTIKI YA KUJIUZULU WALA KUWAJIBISHWA- UJUMBE MFUPI
1. Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), inayoongozwa na Zitto Kabwe hakuniita ili kupata nafasi ya kujitetea, kutokana na shutuma ambazo zimekuwa zikielekezwa kwangu, kwamba nilipewa fedha kupitia akaunti ya Escrow.

2. Kujiuzulu sio fasheni, kwa kuwa fedha nilizopata ni kwa ajili ya mchango wa shule ya Barbro Johansson ya jijini Dar es Salaam na kujiuzulu ni kitu ambacho kina sababu zinazohitaji uwajibikaji. Nijiuzulu kwa kuwa nimepata mchango wa shule?

3. “Nijiuzulu kwa sababu gani?… kwa kupata mchango wa shule!… kujiuzulu ni kitu chenye sababu zake, kujiuzulu sio fasheni, lazima kuwe na sababu, hata Rais aliyenipa kazi atashangaa. Naona ufahari kufanikisha mchango wa shule yangu.

4. Aidha, serikali haijatamka kama James Rugemalira ana fedha haramu na kama fedha hizo, zikitajwa kuwa za haramu, shule yangu itazirudisha, kwa kuwa shule yangu haiwezi kupokea fedha iliyo haramu.

5. “Nilipostaafu kazi UN, Sweden waliniambia kuwa sasa naweza kuendelea kuomba mchango katika nchi yangu na ni kweli kwamba kadri taifa linavyokua wapo watu wenye uwezo na wanaoweza kuchangia katika masuala mbalimbali,” alisema na kuongeza kuwa ndio maana alianza kuomba michango kwa watu mbalimbali wakiwamo wa ndani ya nchi. 
Na kutokana na kuomba mchango, hata Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Reginald Mengi aliwahi kutuchangia Sh milioni 278 kwa kuona umuhimu wa kuendeleza elimu ya mtoto wa kike na mwaka 2012, ndipo nilipomuomba mchango James Rugemalira kupitia kampuni yake ya Mabibo akiwa kama ndugu yake.

6. Nilipomwandikia Rugemalira, alinjibu nitachangiwa, lakini kwa masharti ya kwamba fedha hizo zipitie Benki ya Mkombozi. Na mimi sikuwa na akaunti katika benki hiyo na Februari 23 mwaka huu ndipo nilifungua na haukupita muda mwingi alinipigia na kuniambia kuwa tayari ameshachangia.
 Baada ya kupata mchango huo, niliwapigia viongozi wa Bodi ya shule kuwaeleza kwamba wamepata mchango `babu kubwa’ na alihamisha fedha hizo na kuzipeleka Benki M kwa ajili ya kulipa mikopo ya shule.

7. Profesa Tibaijuka anasema: “Nimejitolea maisha yangu kutafuta wafadhili kwani ada za shule hizo ni kubwa kwani ya Dar es Salaam ni Sh milioni nne na nusu na ile ya Bukoba ni Sh milioni mbili huku pakiwepo pia wanafunzi ambao hawalipi ada wakipatiwa ufadhili.” 
Chanzo: Jiachie Blog

KAGERA KUJIVUNIA UWANJA WA NDEGE WA KISASA

Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango wakiwasili kwenye Kiwanja cha Ndege cha Kagera kujionea maendeleo ya Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja hicho. Waliotangulia mbele ni Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kushoto), Meneja Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Bukoba, Mhandisi Suleiman Athuman (Katikati) na Meneja wa kiwanja hicho, Bw. Julius Mulungwana (Kulia)
Ujenzi unaendelea! Mafundi wakiendelea na ujenzi wa jengo la abiria la Kiwanja cha Ndege cha Kagera.
Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa kiwanja hiko, Mhandisi Pius Gobolo akitoa maelezo ya namna ya kiwanja hicho kitakavyoonekana mara kitakapokamilika. PICHA NA SAIDI MKABAKULI

Na Saidi Mkabakuli, Kagera
Mkoa wa Kagera na maeneo ya jirani wataanza kujivunia uwanja wa ndege wa kisasa kufuatia kukamilika kwa Kiwanja cha Ndege cha Bukoba.
Akizungumza na Wakaguzi wa Miradi ya Maendeleo toka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Meneja Mradi wa Upanuzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kagera, Mhandisi Suleiman Athuman, amesema kwamba maendeleo ya ujenzi wa jengo la abiria la kiwanja hicho upo kwenye hali nzuri na mkandarasi atabidhi kazi hiyo mapema mwakani.
“Katika mwaka wa fedha wa 2013/14 kazi zilizopangwa ni ukarabati na upanuzi wa miundombinu ya kiwanja, ikijumuisha barabara ya kuruka na kutua ndege, maegesho ya ndege, barabara ya kiungio, kwa sasa ujenzi unaendelea vizuri na Mkandarasi atatukabidhi kazi mapema mwakani,” alisema Mhandisi Athuman.
Akitoa taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa Kiwanja cha Bukoba, Mhandisi Mshauri wa ujenzi wa kiwanja hiko, Mhandisi Pius Gobolo amesema kuwa kazi za usimikaji wa mfumo wa taa za kuongozea ndege, ujenzi wa jengo jipya la abiria na uzio wa usalama zimeshakamilika kwa asilimia 80.
“Kama unavyojionea, sehemu kubwa ya kazi imekamilika, kwa makadirio ni zaidi ya asilimia 80 ya ujenzi wa kiwanja hiki imeshakamilika,” aliongeza Mhandisi Gobolo.
Kwa mujibu wa mpangokazi wa ujenzi wa kiwanja hicho hadi kufikia mwezi Juni 2014, hatua iliyofikiwa ni pamoja na kukamilika kwa ukarabati wa barabara ya kuruka na kutua ndege, barabara ya kiungio na maegesho ya ndege kwa kiwango cha lami; na ujenzi wa jingo jipya la abiria kufikia hatua ya usimikaji wa paa na mifumo ya maji safi, maji taka na umeme; na kuendelea kwa ujenzi wa jengo la abiria na kituo cha umeme.
Naye, Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri amesema kuwa Serikali imeazimia kuendelea kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege hususan miradi iliyoibuliwa katika Programu ya Matokeo Makubwa Sasa.
“Kwa mujibu Programu ya Matokeo Makubwa Sasa, serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini ipo kwenye mkakati wa kuuendeleza viwanja vya ndege vyote ili viwe na kiwango kizuri kwa watumiaji wa viwanja hivyo,” alisema Bibi Mwanri.

RC: NATAKA USHINDI KESI FEDHA ZA JK

SERIKALI mkoani Kagera imemtaka mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Colnery Ngudungi kuhakikisha halmashauri hiyo inashinda kesi inayohusu upotevu wa kiasi cha Sh milioni 30.
Fedha hizo ni sehemu ya Sh milioni 150 zilizotolewa na Rais Jakaya Kikwete kwa ajili ya mradi wa maji Kibimba wilayani humo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera John Mongella, alipofanya ziara katika eneo la mradi huo unaojengwa kwa ajili ya matumizi ya maji kwa wananchi wa mji mdogo wa Ngara ikiwemo hospitali teule ya wilaya iitwayo Mulugwanza.
Alitoa kauli hiyo baada ya kupata taarifa kwamba kuna mradi wa maji ambao fedha yake ilitolewa na Rais Kikwete, lakini kuna watu wameuhujumu.
Kutokana na taarifa hiyo, RC huyo aliamua kwenda kukagua mradi huo na kujionea maendeleo yake, ikiwa ni sambamba na kupata maelezo kutoka kwa mkurugenzi wa halmashauri hiyo Ngudungi.
Mkurugenzi alitoa maelezo kwa mkuu huyo wa mkoa ambapo alisema halmashauri hiyo iliomba kiasi cha Sh milioni 200 kwa ajili ya kuboresha miundombimu ya maji mjini Ngara na Rais Kikwete alipofanya ziara wilayani humo mwezi Julai mwaka jana aliahidi kuchangia mradi huo kiasi cha Sh milioni 150.
Alisema Rais alituma kwanza kiasi cha Sh milioni 50 na mara ya pili ilitolewa Sh milioni 100. Alisema fedha hiyo ilitumwa kupitia akaunti ya mamlaka ya maji Ngara jambo lililompa mwanya aliyekuwa Meneja wa mamlaka hiyo, Edward Magai kujichotea kiasi cha Sh milioni 32.
Alisema ili mradi huo ukamilike una unahitaji Sh milioni 43 na baraza la madiwani limeishakaa vikao na kuazimia kuwa hizo fedha zipatikane na kumalizia mradi huo ili kupunguza adha ya ukosefu wa maji katika mji huo ambao wananchi hufuata maji zaidi ya kilometa saba.
Kutokana na maelezo hayo mkuu wa mkoa alitoa agizo halmashauri itafute fedha hizo ili mradi ukamilike lakini pia akaagiza kuhakikisha kesi iliyoko mahakamani halmashauri inashinda.
Chanzo;Habari Leo

KCU WACHAGUA VIONGOZI WAPYA, ‘WATOSA’ WA ZAMANI

CHAMA Kikuu cha Ushirika, Mkoa Kagera (KCU 1990) LTD, kimefanya mabadiliko ya kuwachagua viongozi wapya na kuwatupa wa zamani katika Mkutano Mkuu Maalum.
Uchaguzi huo umefanyika jana chini ya usimamizi wa Mrajisi Msaidizi wa Mkoa Kagera, Rweikiko Shorosi, ambaye alisema serikali inapenda kuona vyama vya ushirika vikifanya vizuri
Alibainisha migogoro inayovikumba vyama vya ushirika vinakwamisha harakati za wananchi kutafuta fursa za kujiwezesha kimaendeleo.
Akisoma majina ya watu waliojitokeza kuchukua fomu  ya kuwania nafasi ya Wajumbe wa Bodi ya KCU 1990, katika Mkutano Mkuu maalum uliofanyika mjini hapa, Shorosi alisema  waliojitokeza kuchukua fomu walikuwa 22
Alisema  majina yaliorudi baada ya kuchujwa ni 18  wote ni sura mpya tofauti na walivyotarajia watu wengi
“Haya majina ndiyo yaliyofikisha asilimia 50 na kuendelea na hivyo, nitasoma majina ya wale waliofuzu vigezo ya kamati iliokaa kuyajadili “alisema.
Katika uchaguzi huo kila Wilaya ilitoa wagombea wa wajumbe wa bodi ambapo katika wilaya za Muleba, Halmashauri ya Bukoba, Missenyi walitoa wagombea zaidi ya wanne huku Manipaa ya Bukoba ikitoa wagombea wawili.
Katika nafasi ya Mwenyekiti wagombea walikuwa wawili ambao ni Frank Muganyizi, aliyepata kura 189 kati ya 246 zilizopigwa na Sylvanus Muhyoza, aliyepata kura 50 hivyo, Muganyizi kutangazwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Bodi hiyo.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilikuwa inawaniwa wajumbe watatu Festo Paulo aliyepata kura 31, Sandru Nyangasha aliyepata kura 78, na Ingatus Batanuzi aliyewashinda kwa kupata kura 136.
Wajumbe wapya wa bodi hiyo waliochaguliwa na Mkutano Mkuu ni pamoja na  Winfrida Kyombo aliyepata kura 102 kutoka Wilaya ya Missenyi na Festo Paulo kura 56, wajumbe kutoka Bukoba mjini ni Sylvanus Muyoza aliyepata kura 227.
Wajumbe kutoka Wilaya ya Muleba ni pamoja na Ignatus Batamuzi aliyepata kura 133, na Projestus Balengela aliyepata kura 44.
Wilaya ya Bukoba waliochaguliwa ni pamoja na sandru Nyangasha aliyepata kura 60 na Frank Muganyizi aliyepata kura 90, pia wajumbe hao walimchagua Dominick Kasaju kutoka Chama cha msingi Bukwali wilayani Missenyi kuwa mwakilishi kutoka nje ya bodi ambapo alipata kura 182.
Akizungumza baada ya uchaguzi huo Mrajis Msaidizi, Moshi Chogero, alisema uchaguzi huo umefanyika kwa mujibu wa sheria namba sita ya mwaka 2013 ni wa uhuru na haki.
Alisema kwa wajumbe ambao walichukua fomu na kujaza lakini majina yao hayakuweza kurudi wanaweza kukata rufaa kwa mrajisi kwani ni haki yao ya kidemokrasi kufanya hivyo.
Chanzo;Tanzania daima

HALMASHAURI ZAAGIZWA KUHAKIKI WAKANDARASI

HALMASHAURI za wilaya zimeagizwa kuunda kamati ndogo kwa ajili kuhakiki wakandarasi waliopewa zabuni za kutengeneza barabara.

Agizo hilo lilitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Enosi Mfuru, katika kikao cha bodi ya barabara kilichofanyika Manispaaa ya Bukoba.

Alisema uhakiki na ukaguzi huo utasaidia kuondoa tatizo la wakandarasi kujenga barabara chini ya kiwango na kulipwa fedha, hali inayochangia kuzisababishia hasara halmashauri na serikali kwa ujumla.

Mfuru alisema ukaguzi huo utasaidia kupunguza malalamiko yaliyoanza kujitokeza kuwa baadhi ya barabara zinatengenezwa chini ya viwango na kusababisha kushindwa kupitika muda mfupi baada ya kutengenezwa.

“Halmashauri zihakikishe kila kijiji kinaweka ulinzi katika barabara hilo, ili kuweza kuzilinda hasa zile za Stabex zilizokuwa zinahudumiwa na jumuiya hiyo kutoka Ulaya, kwani mkataba wake umekwisha zitunzwe kama zamani kabla ya msaada huo,” alisema Mfuru.
Aliwakataza wale ambao wameanza kuchimba madini karibu na barabara hizo, kwani wamekuwa wakisababisha uharibifu wa barabara na kuwataka watafute sehemu nyingine.

Meneja wa TanRoads mkoani hapa, Jonh Kalupale, alisema jumla ya sh bilioni 6 ziliidhinishwa kwa ajili ya matengenezo ya barabara kuu za mkoa katika mwaka wa fedha 2008/09. Kati ya hizo sh bilioni 3.6 ni kwa ajili ya kuhudumia barabara kuu zenye urefu wa kilomita 468.62 na madaraja 126.

Aidha, Kalupale alikiomba kikao hicho kwa kupitia kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa kuwawekea ulinzi wa kutosha makandarasi wanaofanya kazi katika mapori ya Burigi Kasindaga na Kimisi, ili kulinda mali zao na usalama wao kwa ujumla 
 Chanzo;Tanzania Daima

BANDARI YA KASANGA KUANZA KUBORESHWA


Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Watatu kushoto) akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) mara walipowasili katika bandari hiyo kujionea shughuli mbalimbali za maendeleo bandari hapo.
Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) akiwaongoza wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kujionea moja ya meli za kigeni zinazotia nanga katika bandari hiyo. Meli hiyo ni MV Rwegura kutoka nchini Burundi.
 Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) akiwaonesha maghala ya kuhifadhia mizigo katika Bandari ya Kasanga. Maghala hayo yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilali tarehe 22 Februari 2012
 Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) akimfafanualia jambo Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri (Kulia) wakati akimkabidhi taarifa ya maendeleo ya bandari hiyo.
 Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) akitoa ufafanuzi juu ya namna bandari yake inavyohudumia meli kutoka nchi jirani. Wanaomsikiliza ni Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiongozwa na Bibi Florence Mwanri (Kushoto aliyevaa fulana nyeusi).

Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kushoto) akiongea na wakaguzi wa miradi ya maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango kuhusu namna ya kuhudumia meli kutoka nje ya nchi.
 Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa (Kulia) akitoa ufafanuzi juu ya namna bandari yake inavyohudumia meli kutoka nchi jirani. Wanaomsikiliza ni Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiongozwa na Bibi Florence Mwanri (Kushoto aliyevaa fulana nyeusi)
 Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiwa katika picha ya pamoja katika jiwe la msingi la uzinduzi wa maghala ya kuhifadhia mizigo katika Bandari ya Kasanga. Maghala hayo yalifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilali tarehe 22 Februari 2012.
 Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango ikiwa katika picha ya pamoja katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) zilizopo kwenye Bandari ya Kasanga.
---
Na Saidi Mkabakuli, Sumbawanga
Serikali imeazimia kuanza kuiboresha bandari ya kimkakati ya Kasanga inayohudumia nchi za Burundi, Rwanda na Kongo iliyopo katika Ziwa Tanganyika, mkoani Rukwa.
Ahadi hiyo imetolewa na Kiongozi wa Timu ya Ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo kutoka Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri wakati walipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya miundombinu katika Bandari ya Kasanga.
Bibi Mwanri alisema kuwa serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania imepanga kuboresha bandari zote ili kuwa malango kuu la biashara kwa soko la ndani na kwa nchi jirani ili kuongeza uwezo wa kuhudumia shehena kwa ufanisi.
“Tumedhamiria kuendelea kuboresha miundombinu ya bandari hususan miradi iliyoibuliwa katika Programu ya Matokeo Makubwa Sasa ikiwemo Bandari ya Kasanga ili kuweza kukidhi mahitaji ya utoaji wa huduma katika eneo hili,” alisema.
Bibi Mwanri aliongeza kuwa serikali pia imejipanga kuendelea kuboresha miundombinu na ununuzi wa vifaa mbalimbali vya kuhudumia shehena katika bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Kasanga na Kigoma na kukamilisha maandalizi ya ujenzi wa bandari mpya za Mwambani (Tanga), Mbegani (Bagamoyo) na Bandari Kavu ya Kisarawe.
Akizungumza na ugeni huo, Msimamizi Mkuu wa Bandari ya Kasanga, Bw. Mponjoli Thompson Mwamafupa alisema kuwa Bandari hiyo ina fursa nyingi katika kuhudumia shehena na abiria wanaopitia bandarini hapo.
“Bandari yetu ina fursa kubwa za kibiashara kwani tuna wateja wengi kutoka ndani na nje ya nchi wanaotumia bandari yetu kupitishia bidhaa zao, pamoja na abiria wanaosafiri kwenda nje na ndani ya Tanzania,” alisema.
Kwa mujibu wa Mpango wa Maendeleo kwa mwaka ujao wa fedha Serikali imedhamiria kuboresha mazingira yatakayowezesha sekta binafsi kuwekeza katika kujenga miuondombinu na kuboresha usafirishaji wa mizigo katika bandari zote nchini.
Pia, Mpango huo unaweka bayana kuendeleza na ukarabati na ununuzi wa vyombo vya usafiri na usafirishaji katika maziwa.

PIGA KURA ILI TUPATE UZI MPYA WA TIMU YA TAIFA



Watanzania wanatakiwa kupigia kura jezi ya timu ya Taifa ya nyumbani na ugenini kupitia mtandao wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wa www.tff.or.tz ambapo jezi hizo zimewekwa.

TFF ilipokea mapendekezo ya mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa kutoka kwa Watanzania 86. Jezi 11 za nyumbani, bukta nane za nyumbani, jezi nane za ugenini na bukta tano za ugenini ndizo zimepitishwa kwa ajili ya kupigiwa kura.

Mwisho wa kupiga kura ni Desemba 31 mwaka huu. Mpigaji kura anatakiwa kubonyeza kwenye jezi na bukta ambayo ameichagua. Anatakiwa kufanya hivyo kwa jezi ya nyumbani na jezi ya ugenini.

Tunawashukuru wote waliojitokeza kupendekeza mwonekano mpya wa jezi ya timu ya Taifa.


IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)


MUHIMU SANA: FAHAMU JUU YA KUCHANGIA DAMU KWA MAMA MJAMZITO (MASWALI NA MAJIBU) SOMA HAPA



Aina za damu
Aina ya damu (pia huitwa kikundi cha damu) ni uainishaji wa damu kwa kuzingatia kuwepo au kutokuwepo kwa dutu za antijeni za kurithiwa kwenye uso wa chembechembe nyekundu za damu (RBCs). Aina ya damu (Kikundi cha damu) inaamuliwa kwa sehemu, na antijeni za aina ya damu ya ABO zilizo kwenye chembechembe nyekundu za damu.
Aina za damu huathiriwa na huwakilisha michango kutoka kwa wazazi wote wawili. Jumla ya mifumo 30 ya aina ya damu ya binadamu (ikiwa ni pamoja na mifumo ya ABO & Rh) sasa inatambuliwa na Shirika la Kimataifa la Upaji wa Damu (ISBT).
Aina ya damu kamili ni seti kamili ya dutu 30 kwenye uso wa chembechembe nyekundu za damu na aina ya damu ya mtu ni mojawapo ya miungano iwezekanayo ya antijeni za aina ya damu. Katika aina hizo 30 za damu, zaidi ya antijeni 600 tofauti za aina ya damu zimepatikana, lakini nyingi ya hizi ni nadra sana au kwa kiasi kikubwa hupatikana katika makabila fulani.
Mfumo wa ABO ni mfumo muhimu zaidi wa aina ya damu katika 


kuongezewa damu kwa binadamu. Kingamwili kinza-A na kingamwili kinza-B zinazohusika kwa kawaida ni kingamwili za Immunoglobulini M, inayofupishwa IgM. Mfumo wa Rh ni mfumo wa pili muhimu zaidi wa aina ya damu katika kuongezewa damu kwa binadamu ukiwa na antijeni 50 kwa sasa.


Wanawake wengi wajawazito hubeba kijusi kilicho na aina ya damu tofauti na yao na mama huweza kutengeneza kingamwili dhidi ya chembechembe nyekundu za damu za kijusi. Wakati mwingine kingamwili hizi za mama zinaweza kuvuka kondo na kusababisha hemolosia ya chembechembe nyekundu za damu, ambayo inaweza kusababisha ugonjwa wa hemolitiki wa mtoto mchanga (HDN), ugonjwa wa hesabu ya chini ya damu ya kijusi.
Karibu kila mara, mtu ana aina moja ya damu maisha yake yote, lakini mara chache sana aina ya damu ya mtu hubadilika kwa sababu ya kuongezeka au ukandamizaji wa antijeni katika maambukizi, donda ndugu au ugonjwa kinga mwili nafsi.
Aina/Makundi ya damu na Upatanifu wa Chembechembe nyekundu za Damu
  1. Watu wenye damu ya aina ya AB wana antijeni zote mbili za A na B kwenye uso wa chembechembe zao nyekundu za damu na majimaji yao ya damu hayana kingamwili zozote dhidi ya antijeni A au B. Kwa hivyo, mtu mwenye damu ya aina ya AB anaweza kupokea damu aina yoyote (aina ya AB inapendekezwa) lakini anaweza kutoa damu kwa mwingine mwenye aina ya AB pekee.
  2. Watu wenye damu ya aina ya A wana antijeni ya A kwenye uso wa chembechembe zao nyekundu za damu na majimaji yao ya damu yana kingamwili za IgM dhidi ya antijeni ya B. Kwa hivyo, mtu mwenye damu ya aina ya ya A anaweza kupokea damu kutoka kwa watu wenye aina ya A au 0 pekee (aina ya A inapendekezwa) na anaweza kutoa damu kwa watu wengine wenye aina ya A au AB.
  3. Watu wenye damu ya aina ya B wana antijeni ya B kwenye uso wa chembechembe zao nyekundu za damu na majimaji yao ya damu yana kingamwili za IgM dhidi ya antijeni ya A. Kwa hivyo, mtu mwenye damu ya aina ya B anaweza kupokea damu kutoka kwa watu wenye aina ya B au O (aina ya B inapendekezwa) na wanaweza kutoa damu kwa watu wenye aina ya B au AB.
  4. Watu wenye damu ya aina ya O (au kikundi cha damu cha sifuri katika nchi kadhaa) hawana antijeni A au B kwenye uso wa chembechembe zao nyekundu za damu lakini majimaji yao ya damu yana kingamwili kinza-A na kingamwili kinza-B za IgM dhidi ya antijeni za aina ya damu za A na B. Kwa hivyo, mtu mwenye damu ya aina ya 0 anaweza tu kupokea damu kutoka kwa mtu mwenye aina ya 0, lakini anaweza kutoa damu kwa watu wa aina yoyote ya ABO (yaani kundi A, B, AB & O).
Masuala ya kuzingatia kabla ya kuchangia damu kwa mama mjamzito
Kabla ya Kuchangia damu
  1. Zingatia ulaji wa vyakula vyenye madini chuma kama nyama nyekundu (mfano nyama ya ng'ombe), samaki, maharage n.k
  2. Pata chakula bora chenye afya yaani mlo kamili. Epuka vyakula vyenye mafuta hasa vilivyokaangwa.
  3. Kunywa maji mengi angalau glasi 6 hadi 8.
  4. Pata usingizi mzuri wa usiku.
  5. Kumbuka kuwa na kitambulisho chako chochote.
Wakati wakuchangia damu
  1. Vaa nguo inayoweza kukunjwa hadi juu ya kiwiko.
  2. Muonyeshe mtoa damu mkono unaotaka utolewe damu, ikiwezekana muonyeshe na mshipa uliofanikisha kutolewa damu wakati uliopita kama umewahi kuchangia damu.
  3. Kuwa mtulivu wakati wa kutolewa damu ikiwezekana ongea na mchangiaji damu aliyekaribu yako au sikiliza muziki wa taratibu.
  4. Punde umalizapo kuchangia damu, tumia muda wako kufurahia vyakula na vinywaji laini vilivyoletwa na wahamasishaji wa kuchangia damu.
Baada ya kuchangia damu
  1. Kunywa maji mengi zaidi na jiepushe na pombe ndani ya masaa 24 yajayo.
  2. Ondoa bandeji/pamba iliyowekwa pale ulipotobolewa kuzuia damu isitoke baada ya saa 1 baada ya kuchangia damu.
  3. Sehemu iliyochomwa sindano kama bado inatoa damu, izibe kwa nguvu na pamba kavu kisha nyoosha mkono juu kwa dakika 5 hadi 10.
  4. Ili kuepuka maambukizi ya ngozi na muwasho osha kwa maji na sabuni sehemu ya mwili iliyotumika kutoa damu.
  5. Usifanye kazi ngumu yoyote kama kubeba vitu vizito ndani ya siku yote ambayo umetoa damu.
  6. Kama unasikia kizunguzungu na kuishiwa nguvu & pumzi baada ya kuchangia damu unapaswa kukaa chini au kulala hadi utakapojisikia vizuri.
  7. Kula vyakula vyenye protini kwa wingi baada ya kuchangia damu mfano nyama ya ng'ombe, kuku, kunde n.k
Mawali na majibu juu ya Uchangiaji damu
Inachukua muda gani kuchangia damu?
Hatua zote mpaka damu kuwa imetolewa inachukua kama saa moja na dakika 15. Muda mahususi kwa kutoa damu chupa moja ya damu ni dakika 8 hadi 10, ingawa muda hutofautiana kwa sababu tofauti kama hali ya afya ya mchangia damu na mahudhurio ya sehemu za kuchangia damu.
Wakati gani mjamzito hupungukiwa damu?
Upungufu wa damu wakati wa ujauzito unaweza kutokea katika mabidiliko ya kawaida ya ujauzito ambapo chembechembe nyekundu huongezeka kwa kiwango kidogo kuliko maji(Physiological hemodilution), hata hivyo mabadiliko haya yanaweza kurekebishwa kwa kutumia madini chuma na folic acid bila kuhitaji kuongezewa damu. Matatizo yanayoweza kusababisha upungufu mkubwa mpaka kuhitaji kuongezewa ni pamoja na lishe duni(isiyo na madini chuma na vitamin stahiki), maambukizi ya minyoo, malaria, kupasuka kwa mimba iliyotungwa nje ya mfuko wa uzazi (Ruptered Ectopic Pregnancy), kutoka/kutoa mimba, kutokwa damu ukeni kabla, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua.
Mama mjamzito huhitaji kuchangiwa damu wakati upi?
Mama mjamzito huhitaji kuchangiwa damu wakati wowote kabla hajapata matatizo yatakayopelekea kupungukiwa damu. Damu inaweza kuhifadhiwa na kusubiri hali ya dharula ikitokea.
Nini madhara ya mjamzito kupungukiwa damu?
Upungufu wa damu wa muda mrefu unaweza athiri maisha ya mama na mtoto aliyetumboni.Mama anaweza kujikuta moyo ukashindwa kufanya kazi vizuri na kupoteza maisha. Mtoto hataweza kukua vizuri na anaweza fia tumboni au akazaliwa akiwa na uzito mdogo sana.Endapo mjamzito atatokwa na damu nyingi sana ukeni kabla ya kujifungua au baada ya kujifungua anaweza kuishiwa nguvu kabisa, kuzimia au hata kupoteza maisha.
Nini hufanyika baada ya kuishiwa damu?
Mgonjwa hukaguliwa haraka na kujua chanzo cha tatizo lake na kuzuia utokaji wa damu zaidi, huku wakizuia asizimie/kupoteza fahamu kwa kumpatia huduma stahiki ikiwa ni pamoja  kurejesha kiwango cha maji yaliyopungua mwilini haraka sana kwa maji ya drip, wakati jitihada za kutafuta kumwongeza damu zinaendelea.
Wapi watakiwa kwenda kuchangia damu?
Nchini Tanzania, sehemu za kuchangia damu zimegawanyika kikanda kama ifuatavyo :-

(a) Kanda ya Mashariki; inayohudumia mikoa ya Dar es salaam, Morogoro, Dodoma & Pwani. Ofisi kuu za kanda zikiwa Mchikichini, Ilala, Dar es salaam. Simu ni 0715339282.
(b) Kanda ya Ziwa; inayohudumia mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera & Shinyanga. Ofisi kuu za kanda zikiwa Mwanza karibu na Hospitali ya Bugando. Simu ni 0768479381.
(c) Kanda ya Magharibi; inayohudumia mikoa ya Tabora, Kigoma & Singida. Ofisi kuu za kanda zikiwa Tabora karibu na Hospitali ya Kitete. Simu ni 0785733606.
(d) Kanda ya Kusini; inayohudumia mikoa ya Lindi & Mtwara. Ofisi kuu za kanda zikiwa Mtwara karibu na Hospitali ya Ligula. Simu ni0786852051.
(e) Kanda ya Kaskazini; inayohudumia mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Arusha & Manyara. Ofisi kuu za kanda zikiwa Moshi, Kilimanjaro karibu na Hospitali ya KCMC. Simu ni 0716231406.
(f) Kanda ya nyanda za juu Kusini; inayohudumia mikoa ya Mbeya, Iringa & Songea. Ofisi kuu za kanda zikiwa Mbeya karibu na Hospitali ya Meta. Simu ni 0767502430.

Mawali na majibu zaidi juu ya Uchangiaji damu
Swali : Nitalipwa nikichangia damu?
Jibu : Hapana. Hakuna malipo baada ya kuchangia damu. Wachangiaji hutoa damu kwa kujitolea kwa hiari yao.
Swali : Je, ni salama kwa mjamzito kuchangiwa damu?
Jibu : Ni salama kwa kuwa vigezo vyote vya usalama huchukuliwa kwa uzito.
Swali : Je, ni kweli kuwa kila kundi la mchangia damu lazima liwe sawa na mjamzito anayechangiwa?
Jibu : Kwa kawaida damu ya mchangiaji hukusanywa bila kujali ni kundi gani, endapo mjamzito atahitaji kutiwa damu ndipo kundi la damu ya mchangiaji litatafutwa ili kuendana na kundi la mjamzito.
Swali : Kuna faida gani kuchangia damu?
Jibu : Kuokoa maisha, kufahamu kundi lako la damu, kufahamu hali yako ya maambukizi ya magonjwa kama UKIMWI, Kaswende na Mchochota wa aina B & C, pia ni uzalendo.
Swali : Kuna hasara gani anayopata mchangia damu tokana na kuchangia damu?
Jibu : Hakuna hasara anayopata mchangiaji damu kwa kuwa damu atakayochangia itatumika kuokoa maisha ya wenye uhitaji wa damu.
Swali : Je, damu huuzwa kwa wanaohitaji?
Jibu : Hapana, damu haiuzwi na hutolewa bure kwa anaehitaji
Swali : Ni kina nani watakaopata damu niliyochangia?
Jibu : Watu wenye upungufu wa damu hasa watoto, watu waliofanyiwa upasuaji mkubwa, wagonjwa wenye saratani, majeruhi wa ajari na kina mama wajawazito wenye matatizo ya uzazi kama kutokwa damu nyingi baada ya kujifungua.
Swali : Ni magonjwa gani yanaweza kusambazwa kwa njia ya damu?
Jibu : Magonjwa mengi husambazwa kwa njia ya damu kama UKIMWI, Kaswende & Mchochota wa aina B & C na bacteria.
Swali : Je, unaweza kupata maambukizi ya UKIMWI ukichangia damu?
Jibu : Hapana kabisa. Sindano na vifaa vingine vyenye ncha kali vinavyotumika ni safi & salama. Watumishi wa ukusanyaji damu wanafuata viwango vya usalama na kuzuia maambukizi kama walivyofundishwa.
Swali : Je, ni salama kuchangia damu?
Jibu : Ndiyo, ni salama kuchangia damu kwa kuwa kabla ya kuchangia damu mtu hukaguliwa na kuulizwa maswali kuona kama amekidhi vigezo vya kuchangia damu ikiwa ni pamoja na kuangaliwa wingi wa damu na kupimwa shinikizo la damu.
Swali : Ninaweza kuchangia damu ikiwa sijala?
Jibu : Ukichangia damu hujala unaongeza hatari ya kupata matatizo baada ya kuhangia damu, hivyo inashauriwa kula chakula chepesi ndani ya masaa 4 baada ya kuchangia damu.
Swali : Ni damu kiasi gani huchukuliwa kwa wakati mmoja?
Jibu : Ni kiasi cha Mililita 480 za damu ndio kiwango kinachokubaliwa kisheria.
Swali : Ninaweza kutoa damu kila baada ya muda gani?
Jibu : Unaruhusiwa kuchangia damu kila baada ya siku 52 ili kuhakikisha mwili umepata muda wa kutosha kurudisha chembechembe za damu zilizopotea baada ya kuchangia damu wakati uliopita.
Swali : Ninahitaji kula mlo maalumu baada ya kuchangia damu?
Jibu : Hapana, endelea na mlo wako wa kila siku pia unaweza kuhakikisha ni mlo kamili tu.
Swali : Itachukua muda gani kwa mwili kurudisha kiwango cha damu nilichokitoa?
Jibu : Sehemu ya maji (Plasma) ya damu huweza kuridi ndani ya masaa 24 wakati chembechembe za damu hurudi baada ya wiki mbili.
Swali : Je, damu yangu itapimwa magonjwa kama UKIMWI kabla sijatoa?
Jibu : Hapana, hutolazimika kupima UKIMWI kama hauko tayari kufanya hivyo.
Swali : Damu salama ni nini?
Jibu : Damu salama ni  ile imepimwa na kuonekana haina UKIMWI, Kaswende, Mchochota wa aina B & C wala vimelea vya bacteria.
Swali : Nitapata wapi majibu yangu ya vipimo nilivyofanya wakati wa uchangiaji damu?
Jibu : Utapata majibu katika ofisi za damu salama  zilizo karibu nawe au pale ulipochangia damu.
Swali : Nani anaruhusiwa kumchangia damu mama mjamzito?
Jibu : Mtu yoyote mwanamke au mwanaume anaweza kumchangia damu mama mjamzito ikiwa ana afya njema na anajisikia vizuri, umri kati ya miaka 18 hadi 65, uzito usiopungua kilo 50, wingi wa damu zaidi ya gramu 12 kwa desilita, kutokuwa na shinikizo la juu la damu na kwa mwanamke asiwe mjamzito au anayenyonyesha.
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa