MWENGE WA UHURU WAPOKELEWA MKOANI KAGERA NA KUANZA UZINDUZI WA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI YA ZAIDI YABILIONI 12

 Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera Kamishina wa Polisi Diwani Athumani Akishika Mwenge Kutoka kwa Mkimbiza Mwenge Kitaifa Charles F Kabeho Kuashiria Kuwa Mwenge Upo Mkoani Kagera
Kiongozi wa Mbio  za Mwenge wa Uhuru Charles Kabeho Akitoa Ujumbe wa Mbio za Mwenge Nyakabango Wilayani Muleba.
Mkimbiza Mwenge Kitaifa Charles Francis Kabeho Akipima Kuhakikisha kuwa Vipimo Katika Daraja la Kishara  Vipo Sawa
Mkimbiza Mwenge Kitaifa Kiongozi Akizindua Mradi wa Maji Izigo
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Akimpokea Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Mkoani Kagera
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu (Kulia) Akikabidhiwa Mwenge wa Uhuru na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel.
Mradi wa Soko la Ndizi Uliozinduliwa na Mwenge wa Uhuru Wilayani Muleba
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu Kushoto Akimkabidhi Mwenge  wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Luyango Ili Ukimbizwe Wilayani Muleba
Na: Sylvester Rapahel
Mwenge wa Uhuru umepokelewa leo April 8, 2018 Mkoani Kagera na Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel katika Kijiji cha Nyakabango mpakani mwa Geita na Kagera ambapo katika Mkoa wa Kagera Mwenge wa Uhuru utapitia miradi ya maendeleo 65 yenye thamani ya shilingi bilioni 12,385,330,354.
Katika miradi hiyo 65 Mwenge wa Uhuru utazindua miradi 33, utakagua miradi 19, utaweka mawe ya msingi katika miradi 13 aidha,  mchanganuo wa gharama za miradi hiyo 65 itakayopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni kama ifuatavyo, Serikali kuu imechangia kiasi cha shilingi bilioni 5,817,795,968 sawa na asilimia 47%.
Halmashauri za Wilaya zimechangia  kiasi cha shilingi 671,940,497 sawa na asilimia 6%. Aidha wananchi wamechangia shilingi bilioni 2,181,496,962 sawa na asilimia 17%.  Wahisani wamechangia shilingi bilioni 3,714,096,927 sawa na asilimia 30%. 
Mwenge wa Uhuru mwaka huu 2018 umebeba kaulimbiu isemayo “Elimu ni ufunguo wa Maisha; Wekeza Sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu.” Kauli mbiu hii inawahamasisha wananchi hususani wa Mkoa wa Kagera kuwekeza katika elimu kwa kuwapeleka watoto shule ili mkoa wetu na Taifa kwa ujumla lipate wataalam wa kutosha katika kada mbalimbali za kitaaluma na hapo taifa letu litapiga hatua kubwa ya maendeleo kwa kuwatumia wataalamu wetu wa ndani.
Pamoja na Kauli Mbiu tajwa hapo juu Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Mkoa wetu zitaendelea kuwahamasisha wananchi kuhusu Mapambano dhidi ya Rushwa, Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI, Mapambano dhidi ya Matumizi ya Dawa za Kulevya na Mapambano dhidi ya Malaria.
Mara baada ya kupokea Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Kijuu alimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Luyango na Mwenge wa Uhuru ukaanza mara moja mbio zake wilayani humo za kukagua miradi ya maendeleo.
Akitoa ujumbe wa mbio za Mwenge wa Uhuru Kiongozi wa Mbio hizo Charle Francis Kabeho katika eneo la Nyakabango aliwasisitiza wanafunzi kusoma kwa bidii masomo ya Sayansi kwani Serikali imefanya kazi yake ya kujenga shule na vyumba vya mahabara na kuweka vifaa vya kutoasha katika maabara hizo



MKOA WA KAGERA WAVUKA LENGO KATIKA UNDIKISHAJI WA WANAFUNZI AWALI NA DARASA LA KWANZA MWAKA 2018





 
 Pichani juu  ni Shule ya Sekondari Prof Joyce Ndalichako na Wanafunzi wakiwa wanajifunza darasani

Na: Sylvester Raphael
Mkoa wa Kagera wavuka lengo la uandikishaji wa Wananfunzi katika madarasa ya awali na Darasa la kwanza kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Machi 2018 kipindi cha miezi mitatu na ni kipindi ambacho wanafunzi hupokelewa na kuandikishwa shuleni aidha, ifikapo Machi 31 uandikishwaji hukoma rasmi.
Mkoa wa Kagera kwa mwaka 2018 uliotea kuandikisha wanafunzi wa awali 85,553 wavulana wakiwa 42,678 na wasichana 42,875 lakini mkoa umefanikiwa kuvuka lengo kwa kuandikisha  wanafunzi wa Elimu ya Awali 88,343 wavulana wakiwa 44,66o na wasichana 43,683 sawa na asilimia (103.3%).
Elimu ya darasa la kwanza Mkoa wa Kagera ulilenga kuandikisha wanafunzi jumla 89,043 wavulana 44,686 na wasichana 44,357 ambapo mkoa umevuka lengo kwa kuandikisha jumla ya wananfunzi 96,539 wavulana wakiwa 48,244 na wasichana 48,295 sawa na asilimia (108.42%)
Aidha katika hatua nyingine Mkoa wa Kagera umefanikiwa kuandikisha wanafunzi wa kidato cha kwanza kwa asilimia 90.66 na tayari wanafunzi hao wameripoti shuleni na kuanza masomo yao ya sekondari.Wanafunzi waliofaulu na kuchaguliwa kujiunga na Elimu ya Sekondari wavulana walikuwa 17,191 na wasicha 17,971 jumla 35,161.
Wanafunzi walioripoti katika shule za Sekondari Mkoani Kagera hadi kufikia Machi 31, 2018 jumla ni 31,877  sawa na asilimia 90.66 wavulana wakiwa 14,814 sawa na asilimia 86.173 na wasichana 17,063 sawa na asilimia 94.953.
Mkoa unaendelea na juhudi za kuwafuatilia wanafunzi ambao bado hawajaripoti shuleni kuhakikisha wanaripoti mara moja ili kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza. Aidha, uongozi wa Mkoa wa Kagera unatoa rai kwa wazazi na walezi wa wanafunzi ambao bado hawajaripoti shuleni kuhakikisha wanafunzi hao wanaripoti vinginevyo wazazi na walezi watauchukuliwa hatua za kisheria kwa kutowapeleka watoto wao shule.
Vilevile Mkoa wa Kagera unaendelea na juhudi za kuweka mazingira mazuri ya kujifunza na kujifunzia ili kutoa elimu bora kwa wanafunzi. Pia kuhakikisha mkoa unashika nafasi za juu katika mitihani ya kitaifa  na ufaulu wa maksi za juu kama ilivyo desturi ya Mkoa wa Kagera.
 

BAKOBA FC MABINGWA KAMALA CUP 2018, WAIFUNGA IJUGANYONDO BAO 3-0 KWENYE FAINALI UWANJA WA KAITABA


Nahodha wa timu ya Bakoba Fc akiwa amebeba Kombe la Ubingwa leo hii jioni kwenye Uwanja wa Kaitaba mara baada ya kuibuka Kidedea kwa kuifunga Timu ya Ijuganyondo bao 3-0. Katika Mchezo huo Kipindi cha kwanza hakuna Timu iliyopata bao kipindi cha kwanza, Kipindi cha pili goli zote tatu zilipatikana Goli la kwanza likifungwa na Denis Msuva, Bao la pili lilifungwa na Datius Peter na bao la tatu lilifungwa na Ezekiel Izack aliyekuwa amevaa jezi namba 10.
Picha zote na Faustine Ruta, Bukoba.
Picha ya Pamoja ya Mabingwa Bakoba Fc na Mdhamini wa Ligi hiyo ya Kamala Cup 2018 pamoja na Mgeni rasmi na Viongozi wengine.
Mabingwa Bakoba Fc wakiwa wamebeba Mwali wao.
Ligi hii ya Kamala Cup 2018 ilianza Mwezi Februari tarehe 18, 2018 na kushirikisha Timu za Kata 16 na hii leo imehitimishwa kwa Timu ya Bakoba kuibuka Bingwa.
Ndg. Salum Umande Chama akiongozana na  Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo pamoja na mdhamini wa Ligi hii Diwani Kamala Kalumuna (kulia) kwenda Uwanjani kukabidhi Wachezaji zawadi zao. Mshindi wa Kwanza kapata milioni 2 na Nusu, Wa pili kapata milioni 1 na Laki 8 na wa tatu kapata milion moja na Laki mbili.

Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo akitoa neno wakati wa ufungaji wa Ligi hiyo ya Kamala Cup 2018.
Picha zote na Faustine Ruta, Bukoba.
Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo(katikati) ndiye alikuwa mgeni Rasmi katika Fainali hii akiambatana na Diwani Kamala Kalumuna (kulia) ambaye ndiye alikuwa mdhamini wa Ligi hii iliyohitimishwa leo hii na Timu ya Bakoba Kuibuka Kidedea kwa kuifunga Timu ya Ijuganyondo Fc Bao 3-0.  Picha zote na Faustine Ruta, Bukoba.
Viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani wakisalimia Timu Uwanjani.
Viongozi mbalimbali wakiwemo Madiwani wakisalimia Timu Uwanjani.
Viongozi mbalimbali wakishuhudia Timu zote mbili
Timu zote mbili zilisalimiana muda mfupi kabla ya kucheza mchezo huo kati ya Bakoba Fc vs Ijuganyondo Fc kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Kikosi cha Timu ya Bakoba kilichoanza dhidi ya Timu ya Ijuganyondo Fc
Kikosi cha Timu ya Ijuganyondo Fc kilichoanza.
Picha ya Pamoja
Wachezaji wa Timu ya Ijuganyondo wakiomba katikati ya Uwanja muda mfupi na kuanza mchezo huo kwa kasi ambao mpaka kipindi cha kwanza kinamalizika ilikuwa 0-0.
Straika wa Timu ya Bakoba akimiliki mpira wakati wa kipindi cha kwanza cha mchezo huo wa Fainali.
Akiendesha mpira...
Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo(katikati) kulia ni Ndg. Salum Umande Chama wakiwa meza kuu.
Ndg. Salum Umande Chama akiteta jambo na Mgeni rasmi Mkuu wa Wilaya Bukoba Bw. Deodatus Kinawilo meza kuu wakati mtanange unaendelea..
Mwali wa mshindi wa kwanza.
Makombe ya Mshindi wa kwanza, wa pili na Watatu.
Mashabiki waliingia kwa Wingi Uwanjani Kaitaba kushuhudia Fainali hiyo.
Mashabiki waliingia kwa wingi Kaitaba leo.
Mdhamini wa Ligi Mh. Kamala Kalumuna akicheza pamoja na watumbuizaji wa nyimbo mbalimbali wakati wa Mapumziko.
Huku Mashabiki wakimpogeza kwa Ligi hiyo ambayo ilikuwa ikishehenesha Mashabiki kibao Uwanjani hapo Kaitaba. Pia Mdhamini huyo amesema Ligi hiyo ni Endelevu na Mwaka kesho 2019 ataiboresha zaidi ya mwaka huu.
Taswira mbalimbali wakati wa Mtanange huo mkali wa kukata na shaka kati ya Bakoba Fc dhidi ya Ijuganyondo Fc.
Taswira mbalimbali, Kaitaba watu waliingia kwa wingi kushuhudia mtanange huo wa Fainali.
Wakati wa Fainali Kati ya Timu ya Bakoba Fc dhidi ya Ijuganyondo FC
Bao la pili lilipatikana kwa mkwaju wa Penati
Kipa wa Ijuganyondo Fc hakuona ndani...
Mfungaji wa bao la pili Datius Peter akishangilia bao lake kipindi cha pili.
Shangwe!!!
2-0 kiulaini!!!
2-0 Baadhi ya Wachezaji wa Bakoba Fc wakipongezana kwa bao.
3-0 Ezekiel Izack akipongezwa kwa kumwagiwa maji mara baada ya kuipachikia bao la tatu Timu ya Bakoba Fc
Mashabiki mnasemaje?????
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa