PLATINUM CREDIT TANZANIA YACHANGIA MAAFA YA KAGERA




Afisa masoko Platinum Credit Tanzania, Gideon Lufunyo (kushoto) akikabidhi msaada wa mifuko 300 ya saruji ambayo ni sawa na tani 15 kwa Mkuu wa mkoa Kagera, Salum Kijuu ikiwa ni msaada wa taasisi hiyo kwa waathirika wa tetemekonla Ardhi mkoani humo.
Kampuni ya Platnum Credit Tanzania Leo imekabidhi msaada wa mifuko 300 ya sumenti kwa mkuu wa mkoa wa Bukoba Salum Kajuu kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni.

                   
Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Jana ofisa masomo wa kampuni hiyo Gideon Lufunyo alisema  tetemeko hilo limeleta madhara mkubwa ambayo yamewagusa n kwamba nia yao ni kuona shule kinaendelea na ratiba ya kawaida ili watoto wasikose elimu.

STAMICO YACHANGIA MILIONI 20 MAAFA YA TETEMEKO LA ARDHI KAGERA

01
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akizungumza na wawakilishi wa Taasisi mashirika mbalimbali (Hawapo pichani) zilizochangia wanananchi wa Bukoba Mkoani Kagera waliopatwa na maafa ya tetemeko la ArdhiSeptemba 10 mwaka huu ambapo Waziri Mkuu amepokea fedha taslimu sh. milioni 25.62 pamoja na nguo zenye thamani ya sh. milioni mbili kutoka kwa wadau mbalimbali, Huku Shirika la Madini la STAMICO likichangia jumla ya shilingi milioni 20 katika fedha hizo.
Fedha hizo jumla ya shilingi milioni 20 zilizotolewa na STAMICO ni michango ya pamoja iliyotolewa na kampuni tanzu za KTCL, SAMIGOLD na STAMICO yenyewe.
Makabidhiano hayo yamefanyika katika hafla fupi iliyofanyika Ofisini kwa Waziri Mkuu Magogoni jijini Dar es salaam leo.
(PICHA NA JOHN BUKUKU WA FULLSHANGWE-MAGOGONI DAR ES SALAAM)
1
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akizungumza kabla ya kukabidhi msaada wao wa shilingi milioni 20 kwa Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa kulia kwake ni Mahende Michael Peter Mwanasheria Mkuu wa STAMIGOLD na waliosimama nyuma kutoka kushoto ni Raymond Rwehumbiza Mratibu wa mradi Ununuzi wa Madini ya bati KTCL uliopo Kyerwa Mkoa wa Kagera, Alex Rutagwelela Kaimu Mkurugenzi wa Uchorongaji STAMICO , Beatrice Musa Lupi Mhasibu Mkuu STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
2
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akimuonyesha Waziri Mkuu Vocha ya malipo yaliyofanywa kwenye akaunti ya kuchangia wahanga wa Tetemeko la Ardhi Kagera kabla ya kukabidhi rasmi kwa waziri mkuu kutoka kushoto ni Mahende Michael Peter Mwanasheria na Mkuu wa Kitengo cha Sheria STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
3
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Madini nchini STAMICO Bi.Zena Kongoi akikabidhi vocha hiyo kwa Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa kutoka kushoto ni Raymond Rwehumbiza Mratibu wa Ununuzi wa Madini ya KTCL Kyerwa Mkoa wa Kagera, Mahende Michael Peter Mwanasheria na Mkuu wa Kitengo cha Sheria STAMICO na Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO.
4
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa akipiga picha ya pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa STAMICO Bi. Zena Kongoi na ujumbe wake alioongozana nao kutoka shirika hilo.
5 7
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Kassim Majaliwa aki akizungumza jambo na Bi. Koleta Njelekela Meneja Masoko na Uhusiano kwa Umma STAMICO mara baada ya makabidhiano hayo.
8
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Kassim Majaliwa na wageni mbalimbali waliofika ofisini kwake kutoa msaada kwa ajili ya wahanga wa Tetemeko la Ardhi mkoani Kagera wakimkubuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ikiwa ni maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo chake miaka 17 iliyopita.

Waziri mkuu apokea misaada ya waathirika wa tetemeko la ardhi Kagera


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea msaada wa mablanketi kutoka kwa Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.Kulia  ni Mwakilishi Mkuu wa Shirika la JICA nchini Toshio Nagase.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea  hundi ya shilingi milioni 6.7m kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi Taasisi ya wakaguzi wa ndani wa Serikali na kampuni Binafsi Bw.Richard Magongo leo Jijini Dar es Salaam ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea pesa taslimu shilingi milioni 2 kutoka kwa Mwenyekiti wa Magereji Tegeta Bw.Lenard Mwanjela ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 325 kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya ACACIA  ikiwa ni kwa ajili ya  waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea hundi  ya shilingi milioni 41.5 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) Bw.Ayoub Ryoba ikiwa ni kutokana na harambee iliyofanywa na Shirika la Utangazaji  Tanzania(TBC) kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa  akipokea moja ya misaada kutoka kwa Katibu wa Jumuiya ya wafanyabiashara wa kariakoo Bw.Abdallah Mwinyi ambao wametoa vifaa vyenye thamani ya milioni 60 ikiwa ni kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.
Picha na Daudi Manongi
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa