Home » » Waziri mkuu apokea misaada ya waathirika wa tetemeko la ardhi Kagera

Waziri mkuu apokea misaada ya waathirika wa tetemeko la ardhi Kagera


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea msaada wa mablanketi kutoka kwa Balozi wa Japan nchini Masaharu Yoshida ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.Kulia  ni Mwakilishi Mkuu wa Shirika la JICA nchini Toshio Nagase.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea  hundi ya shilingi milioni 6.7m kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi Taasisi ya wakaguzi wa ndani wa Serikali na kampuni Binafsi Bw.Richard Magongo leo Jijini Dar es Salaam ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea pesa taslimu shilingi milioni 2 kutoka kwa Mwenyekiti wa Magereji Tegeta Bw.Lenard Mwanjela ukiwa ni msaada kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea mfano wa hundi ya shilingi milioni 325 kutoka kwa wawakilishi wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya ACACIA  ikiwa ni kwa ajili ya  waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa akipokea hundi  ya shilingi milioni 41.5 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC) Bw.Ayoub Ryoba ikiwa ni kutokana na harambee iliyofanywa na Shirika la Utangazaji  Tanzania(TBC) kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.


Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa Majaliwa  akipokea moja ya misaada kutoka kwa Katibu wa Jumuiya ya wafanyabiashara wa kariakoo Bw.Abdallah Mwinyi ambao wametoa vifaa vyenye thamani ya milioni 60 ikiwa ni kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi Mkoani Kagera.
Picha na Daudi Manongi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa