Home » » SERIKALI KUIJENGA SHULE YA MSINGI ILEEGA NA KUIKABARABTI SHULE YA NYAMILIMA

SERIKALI KUIJENGA SHULE YA MSINGI ILEEGA NA KUIKABARABTI SHULE YA NYAMILIMA


Na Benedict Liwenga-MAELEZO
Serikali imepanga kuijenga shule ya msingi ileega na kufanya ukarabati wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Nyamilima zote zilizopo wilayani kyerwa mkoani Kagera kufuatia uharibifu uliotokana na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani huko mapema mwezi September.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Mhandisi Stella Manyanya alipofanya ziara wilayani huko kuangalia athari za tetemeko katika sekta na elimu.

Mhe. Manyanya alisema kuwa kama serikali imejikita katika kurudisha miundombinu ya umma ikiwemo shule ili kuwawezesha wanafunzi kuendelea na masomo kama kawaida

“Tumeona hali ni mbaya kwenye shule hizi mbili na sisi kama serikali hatuwezi kuliacha suala hili lazima tuzikarabati na kuzijenga zile zinazohitaji kujengwa upya na dhumuni ni kuhakikisha wanafunzi wanaendelea na masomo na kuondokana na changamoto hii: Alisema Mhandisi Manyanya

Aidha Mhandisi Manyanya amemtaka mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Nyamilima kuacha tabia ya kutoa ruhusa hovyo kwa walimu suala ambalo linaathiri taaluma kwa wanafunzi.

Wakati huohuo Mhandisi Manyanya amesema walimu watakaoshindwa kuwawezesha wanafunzi wao kujua kusoma na kuandika watashushwa vyeo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa