NAPE ATENGUA PINGAMIZI LA MADIWANI WA CCM WALIOFUKUZWA BUKUBA


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera jana tarehe 13/08/2013 katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika mjini Bukoba imetangaza uamuzi wake wa kuwafutia dhamana ya CCM hivyo kuwavua Udiwani Madiwani wanane wa Manispaa ya Bukoba waliotokana na CCM.

Kwa mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa viongozi wa CCM walio kwenye vyombo vya dola hasa Wabunge na Madiwani uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Mkoa sio wa mwisho.  Uamuzi huo unapaswa kupata Baraka za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo utekelezwe.

Hivyo basi, mpaka sasa Madiwani hao wanane waliosimamishwa wanapaswa kuendelea na kazi zao kama kawaida wakisubiri kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti, 2013 mjini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kitapitia uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Kagera.

Pamoja na hilo, tumepokea barua za Madiwani hao za kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa kwa msingi wa madai ya kukiukwa kwa utaratibu katika kufikia uamuzi huo.

Tunawasihi wananchi wa Bukoba na Kata husika, wanachama na viongozi wote kuwa watulivu katika kipindi hiki ambapo suala hili linashughulikiwa na vikao vya Kitaifa.

Imetolewa na:-
  
Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
14/08/2013

HOTUBA YA RAIS KIKWETE YA MAJUMUISHO YA ZIARA YA MKOA WA KAGERA MWISHONI MWA JULAI 2013

KAMATI KUU YA CCM KUAMUA HATMA YA MADIWANI BUKOBA


Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kagera jana tarehe 13/08/2013 katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika mjini Bukoba imetangaza uamuzi wake wa kuwafutia dhamana ya CCM hivyo kuwavua Udiwani Madiwani wanane wa Manispaa ya Bukoba waliotokana na CCM.

Kwa mujibu wa utaratibu wa kutoa adhabu kwa viongozi wa CCM walio kwenye vyombo vya dola hasa Wabunge na Madiwani uamuzi wa Halmashauri Kuu ya Mkoa sio wa mwisho. Uamuzi huo unapaswa kupata Baraka za Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ndipo utekelezwe.

Hivyo basi, mpaka sasa Madiwani hao wanane waliosimamishwa wanapaswa kuendelea na kazi zao kama kawaida wakisubiri kikao cha Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa kitakachoketi tarehe 23 Agosti, 2013 mjini Dodoma ambacho pamoja na mambo mengine kitapitia uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa wa Kagera.

Pamoja na hilo, tumepokea barua za Madiwani hao za kukata rufaa kupinga uamuzi huo wa Halmashauri Kuu ya Mkoa kwa msingi wa madai ya kukiukwa kwa utaratibu katika kufikia uamuzi huo.

Tunawasihi wananchi wa Bukoba na Kata husika, wanachama na viongozi wote kuwa watulivu katika kipindi hiki ambapo suala hili linashughulikiwa na vikao vya Kitaifa.

Imetolewa na:-

Nape M. Nnauye,
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA
ITIKADI NA UENEZI
14/08/2013

VYAMA VYA USHIRIKA B'MULO VYAKOSA WAHASIBU WENYE TAALUMA

VYAMA vya ushirika vya kuweka na kukopa katika Halmashauri ya wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera vyadaiwa kushindwa kujiendesha inavyotakiwa kutokana na kukosa wahasibu waliosomea taaluma hiyo.
Ofisa ushirika wa Halmashauri ya wilaya ya Biharamaulo,Mary Kahesi alisema hali hiyo imesababisha vyama hivyo kushindwa kurejesha mikopo ya wanachama na hivyo kukabiliwa na uhaba wa fedha za kuendesha mafunzo kwa wanachama wake.
Kahesi,amesema hayo baada ya kutakiwa na kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bw.Zabron Njanga kutoa maelezo kuhusiana na kuwepo kwa baadhi ya vyama vya ushirika vya vijana kushindwa kurejesha mikopo yake kwa wakati na kupoteza mwelekeo wa mpango  wa kuanzishwa kwake.
Hatua hiyo ya mkurugenzi ilikuja kufuatia baadhi ya madiwani kwenye kikao chao cha baraza kilichofanyika jana(J'tano)kutaka kupewa mpango mkakati wa kuboresha vyama hivyo hasa kwa upande wa makundi ya vijana na akina mama.
Diwani wa kata ya Bisibo Bw.Joseph Kayamba(chadema),alisema pamoja na kuwepo kwa vijana wengi kujiunga kwenye vyama vya ushirika baadhi yao wanakosa mikopo na hivyo vyama hivyo kusambaratika kutokana na kutokuwa na elimu ya ujasiriamali.
Katika taarifa ya utendaji wa kazi na uwajibikaji wa halmashauri hiyo katika kipindi cha kaunzia julai 2012 hadi juni 2013 iliyowasilishwa na ofisa uchumi,Abdalah Mvungi kwenye kikao hicho kuonyesha uhaba wa fedha na wananchi kukosa ubunifu wa kuunganisha shughuli zao ili kuunda vyama vya ushirika.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa