Home » » KCU WACHAGUA VIONGOZI WAPYA, ‘WATOSA’ WA ZAMANI

KCU WACHAGUA VIONGOZI WAPYA, ‘WATOSA’ WA ZAMANI

CHAMA Kikuu cha Ushirika, Mkoa Kagera (KCU 1990) LTD, kimefanya mabadiliko ya kuwachagua viongozi wapya na kuwatupa wa zamani katika Mkutano Mkuu Maalum.
Uchaguzi huo umefanyika jana chini ya usimamizi wa Mrajisi Msaidizi wa Mkoa Kagera, Rweikiko Shorosi, ambaye alisema serikali inapenda kuona vyama vya ushirika vikifanya vizuri
Alibainisha migogoro inayovikumba vyama vya ushirika vinakwamisha harakati za wananchi kutafuta fursa za kujiwezesha kimaendeleo.
Akisoma majina ya watu waliojitokeza kuchukua fomu  ya kuwania nafasi ya Wajumbe wa Bodi ya KCU 1990, katika Mkutano Mkuu maalum uliofanyika mjini hapa, Shorosi alisema  waliojitokeza kuchukua fomu walikuwa 22
Alisema  majina yaliorudi baada ya kuchujwa ni 18  wote ni sura mpya tofauti na walivyotarajia watu wengi
“Haya majina ndiyo yaliyofikisha asilimia 50 na kuendelea na hivyo, nitasoma majina ya wale waliofuzu vigezo ya kamati iliokaa kuyajadili “alisema.
Katika uchaguzi huo kila Wilaya ilitoa wagombea wa wajumbe wa bodi ambapo katika wilaya za Muleba, Halmashauri ya Bukoba, Missenyi walitoa wagombea zaidi ya wanne huku Manipaa ya Bukoba ikitoa wagombea wawili.
Katika nafasi ya Mwenyekiti wagombea walikuwa wawili ambao ni Frank Muganyizi, aliyepata kura 189 kati ya 246 zilizopigwa na Sylvanus Muhyoza, aliyepata kura 50 hivyo, Muganyizi kutangazwa kuwa Mwenyekiti Mpya wa Bodi hiyo.
Nafasi ya Makamu Mwenyekiti ilikuwa inawaniwa wajumbe watatu Festo Paulo aliyepata kura 31, Sandru Nyangasha aliyepata kura 78, na Ingatus Batanuzi aliyewashinda kwa kupata kura 136.
Wajumbe wapya wa bodi hiyo waliochaguliwa na Mkutano Mkuu ni pamoja na  Winfrida Kyombo aliyepata kura 102 kutoka Wilaya ya Missenyi na Festo Paulo kura 56, wajumbe kutoka Bukoba mjini ni Sylvanus Muyoza aliyepata kura 227.
Wajumbe kutoka Wilaya ya Muleba ni pamoja na Ignatus Batamuzi aliyepata kura 133, na Projestus Balengela aliyepata kura 44.
Wilaya ya Bukoba waliochaguliwa ni pamoja na sandru Nyangasha aliyepata kura 60 na Frank Muganyizi aliyepata kura 90, pia wajumbe hao walimchagua Dominick Kasaju kutoka Chama cha msingi Bukwali wilayani Missenyi kuwa mwakilishi kutoka nje ya bodi ambapo alipata kura 182.
Akizungumza baada ya uchaguzi huo Mrajis Msaidizi, Moshi Chogero, alisema uchaguzi huo umefanyika kwa mujibu wa sheria namba sita ya mwaka 2013 ni wa uhuru na haki.
Alisema kwa wajumbe ambao walichukua fomu na kujaza lakini majina yao hayakuweza kurudi wanaweza kukata rufaa kwa mrajisi kwani ni haki yao ya kidemokrasi kufanya hivyo.
Chanzo;Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa