Home » » WADAU WA ELIMU CHATO WALALAMIKIA ELIMU YA AWALI

WADAU WA ELIMU CHATO WALALAMIKIA ELIMU YA AWALI



Watoto wa awali wa shule ya msingi Kalema.
 Watoto wa awali wa shue ya msingi Chato.
-
Na Daniel Limbe,Chato

LICHA ya serikali kuhamasisha
uanzishwaji wa elimu ya awali katika shule zote za msingi hapa nchini
kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kimaarifa watoto
ambao hawajafikia umri wa kuanza elimu ya msingi,hatua hiyo imeonekana
kulalamikiwa sana na baadhi ya wadau wa elimu katika wilaya ya chato
mkoani geita kutokana na kukosekana kwa miundo mbinu mbalimbali ya
kufundishia.

Wakizungumza na mwandishi wa habari
hizi baadhi ya walimu wakuu wa shule za msingi Kalema,Kitela na Chato
wamesema upatikanaji wa elimu ya awali kwa
watoto ni changamoto kubwa kwa serikali kutokana na ukosefu mkubwa wa
vitabu vya kufundishia,vifaa vya kujifunzia na uhaba wa walimu.

Kwa mujibu wa mwalimu mkuu wa shule ya
msingi Chato Mwita Chacha shule yake inawanafunzi wa awali 300 na
kwamba watoto hao wanamwalimu mmoja na kwamba
hakuna madawati ya kukalia wala vifaa vya kujifunzia kwa vitendo hali
inayosababisha watoto wengi kushindwa kupata elimu iliyokusudiwa.

Amesema kitendo cha mwalimu mmoja
kufundisha watoto 300 hakiendani na mpango wa kitaifa wa utoaji elimu
ambao unamtaka mwalimu mmoja kufundisha watoto
40 huku akiiomba serikali kuimalisha miundombinu ya kufundishia
itakayosaidia kuboresha elimu kwa watoto wa shule za awali.

Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule
ya msingi Kalema Tano Bara amesema ili elimu ya awali iweze kupatikana
kwa ufanisi kuna haja kubwa kwa serikali
kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya kununua vitendea kazi vya
kufundishia na kufundishiwa hatua itakayorahisisha upatikanaji wa elimu
bora kwa watoto wa awali ikilinganishwa na hali ilivyo hivi sasa.

Aidha uchunguzi wa Mwandishi wa habari
hizi umebaini aslimia 95 ya shule za awali wilayani chato hakuna vitabu
vya kufundishia watoto badala yake
walimu wa madarasa hayo hulazimika kutumia mihutasari inayotoa miongozo
ya kutolea elimu hiyo huku madawati na vifaa vingine vya kujifunzia
vikionekana kitendawili.

Kutokana na hali hiyo baadhi ya watoto
wa awali imeonekana ni vigumu kwao kujifunza kwa ufasaha kutokana na
baadhi yao kukaa chini na wengine kukalia
mawe wakati wa kujifunza hivyo kusabisha watoto kuwa na miandiko
isiyofaa.

Alipotakiwa kujibu malalamiko hayo
Mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Chato Shaban Ntarambe alidai kuwa
yeye siyo msemaji licha ya kudai kuwa
serikali inayafahamu mapungufu yaliyopo na kwamba taratibu bado
zinafanyika ili kutatua hali hiyo.

Aidha amedai kuwa mwongozo alionao
unamuelekeza kusimamia uandikishwaji wa watoto wa shule za awali kila
kijiji na kwamba hatua zingine zitafuatwa
kulingana na mpango wa serikali.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa