KINANA VISIWANI MULEBA‏

  • Kinana atembelea visiwa vya Iroba,Mazinga na Mulumo
  • Aweka historia ya kuwa Katibu Mkuu wa kwanza kufika kwenye visiwa hivyo
  • Asikitishwa na usumbufu unaofanywa na Sumatra kwa wavuvi
  • Wananchi wamlalamikia kuhusu kujiandikisha kwa mbili,Mkuu wa Mkoa Kagera asema siku ni saba na ndio taarifa ya Serikali na sivinginevyo
  • Wavuvi walalmikia suala la nyavu ,wasema kama ni haramu basi akamatwe anayeziingiza nchini.
  • Kinana awataka viongozi wa CCM Muleba kushikamana na kuwa na umoja kati yao
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto)akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Unenezi CCM Taifa Nape Nnauye (katikati) akati wa safari ya kuelekea kwenye visiwa vya Bumbile ikiwa sehemu ya ziara yakeya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika Wilaya ya Muleba,mkoani Kagera.(Picha na Adam Mzee)
 Sehemu ya Kisiwa cha Bumbile pichani.
 Bango la makaribisho ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasili kwa boti kubwa ya Mv. Safari katika kisiwa cha Bumbile,wilaya ya Muleba mkoani Kagera.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakijaribu viatu vya mtumba kwenye soko la mtumba Iroba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kubeba matofali ya ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi Iroba, iliyopo kisiwa cha Bumbile, Muleba mkoani Kagera.
 Wakazi wa Kata ya Iroba wakiwa wamejikusanya kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka akizungumaz na wakazi wa kata ya Iroba kwenye uwanja wa michezo wa shule ya msingi Iroba.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya Iroba kwenye viwanja vya shule ya msingi Iroba , Bumbile wilaya ya Muleba.(Picha na Adam Mzee)
 Boti ndogo iliyombeba Katibu Mkuu wa CCM,Mbunge wa Jimbo la Muleba ya Kusini Profesa Anna Tibaijuka na Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella kutoka kisiwa cha Bumbile kuelekea Mazinga,wilayani Muleba.(Picha na Adam Mzee)


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiteremka kwa boti katika kisiwa cha Mulumo,wilayani Muleba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipunga mkono wakati akiwasili kwenye kisiwa cha Mulumo.(Picha na Adam Mzee)
 Mbunge wa Muleba Kaskazini ambaye pia ni Naibu Waziri Nishati Charles Mwijageakicheza ngoma wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye kisiwa cha Mulumo, wilayani Muleba mkoani Kagera.(Picha na Adam Mzee)
 Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka akihutubia wakazi wa Muleba mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo Fatuma.(Picha na Adam Mzee)
 Wananchi wa Muleba wakimsikiliza Mbunge wao Profesa Anna Tibaijuka wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM ambaye yupo kwenye ziara ya kujenga na kuimarisha chama.(Picha na Adam Mzee)

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa Muleba mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya michezo Fatuma.(Picha na Adam Mzee)

 Wananchi wa Muleba wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambapo aliwatahadhaisha vijana kuwa makini na makundi ya yanayoundwa na vyama vya upinzani kwani mengi yao yanaelekea kuwa na matendo ya kigaidi.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Muleba mjini kwenye uwanja wa Fatuma ikiwa muendelezo wa ziara yake ya kujenga na kuimarisha chama,Kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi wa CCM.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi kijana Revocatus Mgunda cheti cha kuhitimu udereva wa bodaboda mabpo vijana zaidi ya 360 kutoka wilaya ya muleba wamefuzu mafunzo ya udereva wa boda boda ambayo yalidhaminiwa na mbunge wa jimbo hilo Profesa anna Tibaijuka .(Picha na Adam Mzee)




BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KATIBU MKUU WA CCM KOMREDI KINANA AHANI MSIBA WA MAREHEMU MHE.SAMUEL LUANGISA MJINI BUKOBA LEO‏

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya Marehemu Jaji Mstaafu Samuel Luangisa nyumbani kwake kwa marehemu Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.Marehemu Luangisa ni miongoni  mwa Waasisi wa Taifa na katika vipindi tofauti tofauti alikuwa mkuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi (Kagera),Mbunge na Meya wa Manispaa ya Bukoba pamoja na nyadhifa nyingine.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Jaji Mstaafu Samuel Luangisa mapema leo asubuhi nyumbani kwake kwa Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.
Katibu Mkuu Ndugu Kinana na baadhi ya maofisa wa chama na ndugu na jamaa wa marehemu wakishiriki sala ya pamoja na kumuombea marehemu Mzee Samuel Luangisa nyumbani kwake Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera
Katibu Mkuu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya Marehemu Mh. Samuel Luangisa nyumbani kwake mapema leo asubuhi,Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.

PICHA NA MICHUZI JR-BUKOBA.

KINANA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUWASHABIKIA WAGOMBEA URAIS, BALI WAWAPIME UWEZO WAO

1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akilakiwa na Katibu wa CCM mkoa wa Kagera Bw. Ali Ame wakati alipowasili katika kata ya Nyakanazi wilayani Biharamulo mkoani Kagera wakati akianza rasmi ziara yake ya kikazi ya kukagua na kuhimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali.
Ziara hiyo itafanyika katika mikoa mitatu ya kanda ya ziwa ambayo ni Kagera yenewe, mkoa wa Geita na kisha atamalizia na mkoa wa Mwanza kwa kufanya mkutano mkubwa wa kuhitimisha ziara kutembelea nchi zima ikiwani mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar na majimbo yote ya uchaguzi nchi nzima, ambapo amekutana na wananchi na kusikiliza kero mbalimbali za wananchi, kuzifuatilia na kuzipatia ufumbuzi ,
Wakizungumza katika mkutano wafugaji wa kanda ya Ziwa wamelalamikia wizara ya Maliasili na Utalii hasa askari wa wanyamapori ambapo wamesema wamekuwa wakikamata mifugo yao na kuwatoza faini kuanzia shilingi laki mbili mpaka milioni kumi, Mbaya zaidi wanapodai haki yao wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya kikatili kupita kiasi jambo ambalo linawakatisha tamaa ya maisha kabisa.
Wafugaji hao wameongeza kwamba vikao mbalimbali vimeshafanyika zaidi ya 17 kupitia ngazi zote za kitaifa kasoro kwa Mh. Rais tu ndiyo hatujafika, lakini vikao hivyo vyote havijazaa matunda. bado hali ni mbaya na manyanyaso yanazidi kuendelea, wamemuomba Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kuwasaidia ili waweze kupata ufumbuzi wa suala hilo na wao waweze kuishi na kufanya shughuli zao kwa amani.
Katika ziara zake hizo Kinana amekuwa akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi wa CCM Ndugu Nape Nnauye. (PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-KAGERA)
3
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM wakisalimiana na viongozi mbalimbali mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo.
4 6
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa skafu mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo.
7
Baadhi ya viongozi wakifurahia ujio wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo. 8
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na viongozi mbalimbali na wananchi mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo.
9 10
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Nape Nnauye wakisalimiana na wananchi mbalimbali mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo.
11
Mtoto akiwa amembeba mtoto mwenzake wakati wa mapokezi hayo
12
Ali Ame katika wa CCM mkoa wa Kagera akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
14
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi mbalimbali mara baada ya kulakiwa katika kata ya Nyakanazi Wilayani Biharamulo leo.
15
Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Kinana mara baada ya kumpokea katika mji wa Nyakanazi.
16
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Kanda ya Ziwa Bwa.Mugisha Mushad wakati alipokuwa akitoa malalamiko ya wafugaji kwa ukatili wanaofanyiwa na askari wa wanyamapori katika mapori mbalimbali ya hifadhi kanda ya ziwa.
17
Baadhi ya wafugaji wakimsiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati alipokuwa akizungumza nao katika mji wa Nyakanazi.
18
Katibu Msaidizi Chama cha Wafugaji Kanda ya Ziwa Bwa. Khamis Biteko akitoa ushuhuda wa manbo wanayofanyiwa wafugaji hao na askari wa wanyamapori wakati wa mkutano huo.
20
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wafugaji wa Kanda ya Ziwa wakati walipokutana naye katika mji wa Nyakanazi wilayani Biharamulo na kutoa kero zao kwake juu ya manyanyaso wanayofanyiwa na askari wa wanyamapori.
21
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Kanda ya Ziwa Bwa.Mugisha Mushad wakati alipokuwa akinuobyesha eneo linalotumika kuhifadhi mifugo yao mara inapokamatwa eneo hilo ni dogo na halina chakula cha mifugo wala maji jambo ambalo linafanya mifugo kufa kwa wingi ikiwa imekamatwa.
22
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akionyeshwa eneo hilo na wananchi mbalimbali wakati alipotembelea na kujionea eneo hilo.
23
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akielekea kuwasalimia wananchi wa katika kijiji cha Kyamyorwa.
24
Nape Nnauye akizungumza na wananchi katika kijiji cha Kyamyorwa wakati msafara wa Katibu Mkuu uliposimama kuwasalimia wananchi hao.
26
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akilimiana na wananchi wa kijiji cha Kyamyorwa .
27
John Mongela mkuu wa mkoa wa Kagera akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Kyamyorwa.

REGISTRATION IS NOW OPEN FOR IMPACT ASSESSMENT EVALUATION SHORT COURSE‏

Untitled
Venue – ESRF Conference Hall
Date - 1st-5th June 2015
Course Objective:
This course on Impact Assessment Evaluation will provide researchers, project managers, policy makers, and practitioners of development with the necessary methodology and practical knowledge to meet the growing demand for rigorous evaluation of development programmes.
Learning Outcome
In this course you will learn how to design an impact evaluation of a development intervention employing both quantitative and qualitative methods. Some of the questions you will be able to answer include:
How do we frame the right evaluation questions and choose the right indicators?
What are the best impact evaluation methodologies?
How do we go beyond simple impact assessment by assessing spill-over effects, cost-effectiveness and impact on vulnerable groups?
What are cutting-edge qualitative and quantitative methods for impact assessment?
Should there be any interest from you or your organization email us on trainings@esrf.or.tz by Wednesday 27th May 2015.
Thank you for your valuable time it is much appreciated.

BODI YA WAKURUGENZI YAANZA ZIARA MIKOANI KUKAGUA MIRADI YA UJENZI WA NYUMBA ZA NHC‏

 New Picture
Makamu  Mwenyekiti  wa  Bodi  ya  NHC Bw. Diotrephes  Mmari  na baadhi  ya  Wakurugenzi  wa Bodiya NHC wakikagua ubora wa  vifaa vya ujenzi  vinavyotumika katika ujwenzi wa jingo la kibiashara linalojengwa  na NHC eneo la Mtukula  mpakani mwa Tanzania na Uganda. Wamefurahishwanakazinzurinauborawaujenziwajengohilo la kibiashara na kuwataka wakandarasi wazingatie ubora katika kujenga jengo hilo.Katika  ziara hiyo yupo Mkurugenzi wa BodiBw. Samson Kassalana Charles Mafurua mbaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Nyumba, katika Wizaraya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.
New Picture (1)
Makamu  Mwenyekiti  wa Bodi ya  NHC Bw. Diotrephes  Mmari  na baadhi  ya  Wakurugenzi  wa  Bodiya NHC wakiendelea kukagua jingo la kitegauchumi  linalojengwana NHC eneo la Mtukula  Kagera.
New Picture (2)
Meneja Mkoa wa NHC Kagera Bw. Ng’aranga Magai akito ataarifa ya utekelezaji kwa Makamu  Mwenyekiti wa Bodi  ya NHC   Bw. Diotrephes  Mmari  na baadhi  ya Wakurugenzi wa Bodiya NHC muda mfupi baada ya Bodi hiyo kutembelea mradi wa ujenzi wajengo la biashara linalojengwa na  Shirika  eneo la Mtukula  Mkoani humo.
New Picture (3)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na baadhi ya Wakurugenzi wa Bodi ya NHC walipowasili kukagua mradi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC Wilayani Muleba ambazo ziko katika hatua ya mwisho ya kukamuilika.
New Picture (4)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari akitoa maelekezo kadhaa kwa watendaji wa NHC alipotembelea mradi wa nyumba za kuuza za bei nafuu zinazojengwa na NHC Wilayani Muleba.
New Picture (5)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakikagua nyumba za malazi za NHC zilizopo Wilayani Chato muda mfupi baada ya kuwasili ukitokea Muleba kukagua mradi wa nyumba za gharama nafuu uliojengwa Wilayani humo na Shirika.
New Picture (6)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakiendelea kukagua nyumba za makazi za NHC Wilayani Chato na kusikiliza baadhi ya wapangaji wa nyumba hizo za ghorofa.
New Picture (7)
Msimamizi wa mradi wa nyumba za gharama nafuu zilizojengwa na NHC eneo la Bombambili Geita Injinia Julius Ntoga akitoa maelezo ya hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo ambao umeshakamilika kwa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya NHC. Mradi huo uko katika hatua za mwisho za kukamilika.
New Picture (8)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakiendelea kukagua mradi wa nyumba za gharama nafuu unaotekelezwa na NHC Mkoani Geita.
New Picture (9)
Meneja wa NHC Mkoani Mwanza Injinia Benedict Kilimba akitoa maelezo ya jengo kubwa kuliko yote la kitegauchumi linalotarajiwa kujengwa Jijini Mwanza kwa ushirikiano wa NHC na Benki ya Rasilimali (Investment Bank) kwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake.
New Picture (10)
Makamu Mwenyekiti wa Bodiya NHC Bw. Diotrephes Mmari na Wajumbe wengine wa Bodi ya Wakurugenzi wakiwasili eneo la Buswelu Jijini Mwanza kukagua utekelezaji wa ujenzi wanyumba za gharama nafuu unaofanywa na Kampuni ya Kiure Investment kama mkandarasi mzawa. Wajumbe wa Bodi hiyo wamesikitishwa na hatua ya mamlaka za maji, umeme na barabara kuacha jukumu lao la msingi la kuweka huduma hizo katika miradi ya nyumba inayojengwa na NHC hali inayoongeza gharama. Wameahidi kulisukuma jambo hilo kwenye mamlaka  husika ili zitekeleze jukumu lao.
New Picture (11)
Ujumbe wa Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. DiotrephesMmari ukiendelea kukagua nyumba za gharama nafuu eneo la Buswelu ambapo wamemtaka mkandarasi kuzingatia viwango na ubora katika ujenzi ili wakandarasi wazawa waendelee kuaminiwa na Shirika.
New Picture (12)
Ni eneo la Buhare katika Manispaa ya Musoma ambalo linajengwa nyumba za gharama nafuu na NHC kwaajili ya kuuza. Hapa  NHC Bw. Diotrephes Mmari naWajumbe wengine wa Bodi yaWakurugenzi akiwemo Samson Kassalana Charles Mafuru wanakagua utekelezaji wa mradi huo.
New Picture (13)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakihitimisha kukagua mradi wa nyumba za gharama nafuu zinazojengwa na NHC eneo la BuhareManispaa ya Musoma.
New Picture (14)
Makamu Mwenyekiti wa Bodiya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakikagua jengo la biashara la Mukendo Commercial Complex lililojengwana NHC Mjini Musoma ambalo limeshakamilika na kupangishwa kwa wafanyabiashara ikiwemo benkiya NMB.
New Picture (15)
Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya NHC Bw. Diotrephes Mmari na ujumbe wake wakiwendelea kukagua eneo la ghorofa za juu katika jengo la NHC Mukendo Commercial complex, Mjini Musoma.
New Picture (16)
Makamu Mwenyekiti wa Bodiya NHC Bw. Diotrephes Mmari akiongea na wafanyakazi wa NHC Mkoawa Mara katika Hoteli ya Setavila Mjini Musoma nakusisitiza nidhamu na uadilifu katika utumishi wao ndani ya Shirika.

ANASWA AKIIBA MAHINDI, ALAZIMISHWA KULA MABICHI!

Akilazimishwa kula maindi hayo.
Akila maindi hayo ili kuepuka kichapo.


HAMIDA HASSAN
Jamaa ambaye jina halikuweza kupatikana mara moja, amejikuta akionja joto ya jiwe baada ya kudaiwa kukutwa akiiba kwenye shamba la mahindi hivyo kulazimishwa kula mahindi mabichi.Tukio hilo la aina yake lilijiri hivi karibuni kwenye Kata ya Miembeni, Bukoba mkoani Kagera na kuibua gumzo kubwa.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu, baada ya kumnasa kijana huyo akiiba mahindi aliyoyajaza kwenye gunia, wamiliki wa shamba hilo walimuamuru kukaa chini na kuyala yakiwa mabichi hadi yaishe, kitendo ambacho jamaa huyo alikubaliana nacho.

lielezwa kwamba, katika hali ya kushangaza, kijana huyo hakukataa wala kuonesha kutetereka kwani alianza kuyala hadi alipoamriwa kuacha na kuambiwa aondoke.Katika habari hiyo iliyoripotiwa na Mtandao wa Harakati, kijana huyo alionekana kuwa na matatizo ya kutosikia vizuri wala kuongea kwa maana ya kuwa ni ‘bubu’.

Hata hivyo, kijana huyo hakujulikana alitokea wapi kwani mbali na madai ya wizi na ububu pia hakuonekana mwenye ufahamu mzuri kutokana na mavazi aliyokuwa amevaa. GPL
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa