Home » » ziara ya kinana ngara‏

ziara ya kinana ngara‏

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimia wananchi wa Benaco waliojitokeza kumpokea alipowasili wilayani Ngara kwa ziara ya kukagua, kuhimiza na kusimamia utekelezaji wa ilani ya Uchaguzi.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye akisalimia wakazi wa Benaco wilayani Ngara.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimpatia chanjo mmoja wa watoto katika kituo cha afya cha Nyakisasa, Kashinga wilayani Ngara.
 Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella akizungumza mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana(kulia) kuzindua chanjo kwa watoto wadogo walio chini ya miaka 5 ambapo watoto wamekuwa wakipewa chanjo ya Vitamini A na chanjo ya Minyoo, Mkuu wa mkoa amehimiza Mama wajawazito pamoja na wenye watoto wasiozidi miaka 5 kuhakikisha wanapata chanjo kwa wakati.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza mara baada ya kuzindua chanjo kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano katika kituo cha afya cha Nyakisasa, Kashinga wilayani Ngara.



 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kupanda mti kama ishara yautunzaji mazingira mara baada ya kuzindua chanjo katika kituo cha afya cha Nyakisasa, Kashinga wilayani Ngara mkoani Kagera.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishirikiana na baadhi ya viongozi wa CCM wilaya ya Ngara kuezeka bati katika ofisi ya Tawi la CCM Munjebwe,Ngara mkoani Kagera.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya  Rulenge, Ngara mkoani Kagera.
 Wananchi wa kata ya Rulenge wakisikiliza houba za viongozi kwa makini kwenye mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa kata ya Rulenge wilayani Ngara mkoa wa Kagera.

 Kadi za wanachama waliorudi CCM kata ya  Rulenge ,Ngara mkoani Kagera mara baada ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kumaliza kuhutubia.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipata maelezo juu ya mradi wa umeme Djuruligwa alipoutembelea wilayani Ngara, mkoa wa Kagera.
 Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe.John Mongella akizungumza na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya kumaliza kuutembelea mradi wa umeme Djuruligwa, katikati ni Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka nje ya jengo maalum la kuendeshea pampu za maji katika mradi wa maji Ngara mjini.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipiga ngoma za asili mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa mikutano Posta ya Zamani ,Ngara mkoani Kagera.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipita kuona na kusabahi vikundi vya ngoma za asili na wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa mkutano Posta ya Zamani Ngara.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake mkoa wa Kagera Revina Jovin akiwasalimu wananchi waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara wa CCM kwenye viwanja vya Posta ya Zamani Ngara ambapo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni rasmi.
 Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Kagera Ndugu Yahya Kateme akisalimu wananchi wa Ngara kwenye viwanja vya Posta ya Zamani kwenye mkutano wa hadhara wa CCM ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni rasmi.
 Wananchi wa Ngara mjini wakimkaribisha Kinana kwenye uwanja wa mkutano.

Mkuu wa Wilaya ya Ngara Ndugu Costantine Kanyasu akisalimia wananchi kwenye mkutano hadhara ambao Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana alikuwa mgeni wa heshima.

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa Ngara mjini ambapo alisisitiza kuwa umoja na mshikamano ndani ya CCM ndio nguzo kuu ya uhai wa chama na pia alisisitiza Siasa isichanganywe na Dini hasa pale yanapozungumziwa mambo ya msingi kama Katiba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa Ngara mjini kwenye viwanja vya mkutano Posta ya Zamani ambapo aliitaka serikali kusegeza huduma karibu na jamii badala ya mtu kufunga safari kutoka Ngara kwenda Bukoba mjni kufuata leseni za biashara ama za udereva,Katibu Mkuu aliwahakikishia wananchi wa Ngara kuwa CCM itashinda vizuri na ushindi mkubwa katika uchaguzi mkuu mwezi oktoba mwaka huu.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihojiwa na vyombo vya habari mara baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara Ngara mjini.
 Wananchi wakimuuliza masali Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana mara baada ya mkutano kumalizika.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiagana na wananchi wa Ngara mjini mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara.
(Picha zote na Adam Mzee)

BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa