Home » » KINANA AMALIZA ZIARA JIMBO LA BUKOBA VIJIJINI LEO, KESHO KUENDELEA MISENYI‏

KINANA AMALIZA ZIARA JIMBO LA BUKOBA VIJIJINI LEO, KESHO KUENDELEA MISENYI‏

1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto , Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh. Jason Rweikiza katikati na Novatus Nkwama Mwenyekiti wa CCM Bukoba Vijijini wakishiriki kufukia mabomba katika mradi wa maji unaotekelezwa na serikali katika kata ya Ibyera Bukoba vijijini wakati Katibu Mkuu huyo akiendelea na ziara yake katika jimbo hilo leo, Katibu Mkuu huyo yuko katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Kagera , Geita na Mwanza akikagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 huku akihimiza uhai wa Chama akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BUKOBA VIJIJINI)
4
Wananchi mbalimbali wakimsubiri Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku mabango makubwa yanayoonyesha picha za viongozi wa hao yakiwa yamewekwa katika kijiji hicho wakati alipowasili katika Kata ya Rukoma kwa ajili ya kuzungumza na wananchi.
5
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh John Mongela kushoto wakiwasili katika eneo la mkutano wa hadhara uliofanyika latika kata ya Rukoma.
6
Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mkoani Kagera Mh. Jason Rweikiza akizungumza na wananchi katika kata ya Rukoma Bukoba vijijini wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika jimbo hilo.
7
Baadhi ya watoto wakiushangaa msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati ulipowasili katika kata ya Rukoma.
8
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa ameshikana mikono na Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh. Jason Rweikiza , Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Costansia Buhiye na viongozi wa kata wakati wenyeviti hao wa CCM kata za Bukoba Vijijini walipokabidhiwa baiskeli zilizotolewa na Mbunge huyo kwa watendaji wa Chama cha Mapinduzi Bukoba vijijini.
9
Bw. Pius Rugonzibwa Mmoja wa waandishi wa habari waliokatika msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amesimama juu ya kilima huku akiwa amenyanyua juu kompyuta mpakato yake wakati akijaribu kutuma habari katika kijiji cha Rukoma ambachi pia kina tatizo kubwa la mnara wa mawasiliano jambo ambalo Kinana amelichukua na kuahidi kulifanyia kazi ili kata hiyo ipate mawasiliano ya simu na mtandao.
14
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia Katorowananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
15 16
Umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo uliofanyika kwenye kata ya Katoro.
17 19
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
20
Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh Jason Rweikiza akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
21
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Ndugu John Mongela akizungumza na wananchi na kuwaambia asiwatishe mtu nendeni mkatumie haki yenu ya kikatiba mkajiandikishe katika daftari la wapiga kura katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
22
Baadhi ya wananchi wakinyanyua mikono yao juu kuashiria kukubaliana na mambo mbalimbali yaliyozungumzwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani katika kata ya Rukoma.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa