KOMREDI KINANA AZIDI KUCHANA MBUGA, ATUA KYERWA, KAGERA‏


 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitembelea shamba la mkulima bora wa migomba, Eurius Kishinju katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa, mkoani Kagera. Kinana ambaye ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye wanaanza rasmi ziara mkoani Kagera, ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi

Kishinju ambaye ana shamba la migomba heka 3 mchanganyiko na kahawa, kwa mwezi huuza mikungu 43 kwa mwezi ambapo kila mkungu huuza kwa sh. 10,000, hivyo kujipatia kitita cha sh. 430,000, pia hvuna magunia 25 ya kahawa, ambapo sehemu ya mapoato hayo amejengea nyumba ya kisasa na kusomesha watoto wake wawili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Dodoma.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Komredi Kinana akioneshwa zao la kahawa alipotembelea shamba hilo
 Komredi Kinana akikagua shmba bora la migomba na kahawa katika Kata ya Mabira, linalomilikiwa na mkulima Kishinju
 Wananchi wa Kata ya Nkwenda wakimpigia makofi Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana alipokuwa akihutubia katika Kijiji cha Nkwenda, wilayani Kyerwa, ambapo aliahidi kufikisha kilio cha bei ndogo ya kahawa katika vikao vya ngazi ya juu na hasa Kamati Kuu ya CCM Julai mwaka huu, ili wakulima wa zao hilo waruhusiwe kuuza watakako kwenye bei kubwa.
 Katibuwa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Kikukuru, Katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa. Mabira Kikukuru
 Wananchi wakishangilia wakati wa mkutano huo
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa, mkoani Kagera
Wananchi wakimsalimia Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana alipokwenda kukagua  Zahanati yaKijiji cha Kigorogoro wilayani Kyerwa, Kagera.
 Wananchi wakiwa na furaha wakati wa kumlaki Komredi Kinana katika Kijiji cha Kigorogoro, wilayani Kyerwa
 Komredi Kinana akihutubia alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Soko la Kimataifa la Murongom wilayani Kyerwa, ambao hivi sasa umesimama.Soko hilo lipo mpakani mwa Tanzania na Uganda.
 Wananchi bwa Kata ya Kaisho, Kijiji cha Kibingo wakishangilia walipokuwa wakimlaki Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana ambaye alifanya ziara katika eneo hilo kuzindua mradi wa maji na kuhutubuia wananchi.

 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, ,AKIWA AMESIMAMA KWENYE GARI AKIANGALIA MWENENDO WA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KIJIJI CHA KIBINGO, WILAYANI KYERWA.
 Komredi Kinana akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kibingo, Kata ya Murongo.
 Wananchi wakiwa na hamu ya kumsalimia alipowasili katika Mji wa Isingiro,Makao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera.
 Komredi Kinana akisalimiana na wananchi katika Mji wa Isingiro, wilayani Kyerwa, Kagera.
 Ni furaha iliyoje kwa wakazi wa Mji wa Isingiro walipokuwa wakimlaki, Komredi Kinana
 Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, Kategile akielezea miradi mbalimbali aliyoitekeleza jimbo humo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wakati wa mkutano huo wa hadhara
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Napoe Nnauye akihutubia katika mkutano huo.

KINANA AMALIZA ZIARA JIMBO LA BUKOBA VIJIJINI LEO, KESHO KUENDELEA MISENYI‏

1
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kushoto , Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh. Jason Rweikiza katikati na Novatus Nkwama Mwenyekiti wa CCM Bukoba Vijijini wakishiriki kufukia mabomba katika mradi wa maji unaotekelezwa na serikali katika kata ya Ibyera Bukoba vijijini wakati Katibu Mkuu huyo akiendelea na ziara yake katika jimbo hilo leo, Katibu Mkuu huyo yuko katika ziara ya kikazi katika mikoa ya Kagera , Geita na Mwanza akikagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 huku akihimiza uhai wa Chama akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-BUKOBA VIJIJINI)
4
Wananchi mbalimbali wakimsubiri Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku mabango makubwa yanayoonyesha picha za viongozi wa hao yakiwa yamewekwa katika kijiji hicho wakati alipowasili katika Kata ya Rukoma kwa ajili ya kuzungumza na wananchi.
5
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mh John Mongela kushoto wakiwasili katika eneo la mkutano wa hadhara uliofanyika latika kata ya Rukoma.
6
Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mkoani Kagera Mh. Jason Rweikiza akizungumza na wananchi katika kata ya Rukoma Bukoba vijijini wakati wa Ziara ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika jimbo hilo.
7
Baadhi ya watoto wakiushangaa msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati ulipowasili katika kata ya Rukoma.
8
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa ameshikana mikono na Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh. Jason Rweikiza , Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera Costansia Buhiye na viongozi wa kata wakati wenyeviti hao wa CCM kata za Bukoba Vijijini walipokabidhiwa baiskeli zilizotolewa na Mbunge huyo kwa watendaji wa Chama cha Mapinduzi Bukoba vijijini.
9
Bw. Pius Rugonzibwa Mmoja wa waandishi wa habari waliokatika msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amesimama juu ya kilima huku akiwa amenyanyua juu kompyuta mpakato yake wakati akijaribu kutuma habari katika kijiji cha Rukoma ambachi pia kina tatizo kubwa la mnara wa mawasiliano jambo ambalo Kinana amelichukua na kuahidi kulifanyia kazi ili kata hiyo ipate mawasiliano ya simu na mtandao.
14
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia Katorowananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
15 16
Umati wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo uliofanyika kwenye kata ya Katoro.
17 19
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM akihutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
20
Mbunge wa jimbo la Bukoba Vijijini Mh Jason Rweikiza akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
21
Mkuu wa Mkoa wa Kagera Ndugu John Mongela akizungumza na wananchi na kuwaambia asiwatishe mtu nendeni mkatumie haki yenu ya kikatiba mkajiandikishe katika daftari la wapiga kura katika kata ya Katoro Bukoba Vijijini.
22
Baadhi ya wananchi wakinyanyua mikono yao juu kuashiria kukubaliana na mambo mbalimbali yaliyozungumzwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani katika kata ya Rukoma.

KINANA VISIWANI MULEBA‏

  • Kinana atembelea visiwa vya Iroba,Mazinga na Mulumo
  • Aweka historia ya kuwa Katibu Mkuu wa kwanza kufika kwenye visiwa hivyo
  • Asikitishwa na usumbufu unaofanywa na Sumatra kwa wavuvi
  • Wananchi wamlalamikia kuhusu kujiandikisha kwa mbili,Mkuu wa Mkoa Kagera asema siku ni saba na ndio taarifa ya Serikali na sivinginevyo
  • Wavuvi walalmikia suala la nyavu ,wasema kama ni haramu basi akamatwe anayeziingiza nchini.
  • Kinana awataka viongozi wa CCM Muleba kushikamana na kuwa na umoja kati yao
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto)akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Unenezi CCM Taifa Nape Nnauye (katikati) akati wa safari ya kuelekea kwenye visiwa vya Bumbile ikiwa sehemu ya ziara yakeya kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika Wilaya ya Muleba,mkoani Kagera.(Picha na Adam Mzee)
 Sehemu ya Kisiwa cha Bumbile pichani.
 Bango la makaribisho ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana pamoja na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakiwasili kwa boti kubwa ya Mv. Safari katika kisiwa cha Bumbile,wilaya ya Muleba mkoani Kagera.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye wakijaribu viatu vya mtumba kwenye soko la mtumba Iroba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kubeba matofali ya ujenzi wa madarasa ya shule ya msingi Iroba, iliyopo kisiwa cha Bumbile, Muleba mkoani Kagera.
 Wakazi wa Kata ya Iroba wakiwa wamejikusanya kumsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka akizungumaz na wakazi wa kata ya Iroba kwenye uwanja wa michezo wa shule ya msingi Iroba.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia wakazi wa kata ya Iroba kwenye viwanja vya shule ya msingi Iroba , Bumbile wilaya ya Muleba.(Picha na Adam Mzee)
 Boti ndogo iliyombeba Katibu Mkuu wa CCM,Mbunge wa Jimbo la Muleba ya Kusini Profesa Anna Tibaijuka na Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella kutoka kisiwa cha Bumbile kuelekea Mazinga,wilayani Muleba.(Picha na Adam Mzee)


 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiteremka kwa boti katika kisiwa cha Mulumo,wilayani Muleba.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipunga mkono wakati akiwasili kwenye kisiwa cha Mulumo.(Picha na Adam Mzee)
 Mbunge wa Muleba Kaskazini ambaye pia ni Naibu Waziri Nishati Charles Mwijageakicheza ngoma wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana kwenye kisiwa cha Mulumo, wilayani Muleba mkoani Kagera.(Picha na Adam Mzee)
 Mbunge wa Muleba Kusini Profesa Anna Tibaijuka akihutubia wakazi wa Muleba mjini kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo Fatuma.(Picha na Adam Mzee)
 Wananchi wa Muleba wakimsikiliza Mbunge wao Profesa Anna Tibaijuka wakati wa mkutano wa hadhara wa Katibu Mkuu wa CCM ambaye yupo kwenye ziara ya kujenga na kuimarisha chama.(Picha na Adam Mzee)

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiwasalimu wakazi wa Muleba mjini waliojitokeza kwa wingi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya michezo Fatuma.(Picha na Adam Mzee)

 Wananchi wa Muleba wakimsikiliza Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye ambapo aliwatahadhaisha vijana kuwa makini na makundi ya yanayoundwa na vyama vya upinzani kwani mengi yao yanaelekea kuwa na matendo ya kigaidi.(Picha na Adam Mzee)
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Muleba mjini kwenye uwanja wa Fatuma ikiwa muendelezo wa ziara yake ya kujenga na kuimarisha chama,Kukagua utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi wa CCM.

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimkabidhi kijana Revocatus Mgunda cheti cha kuhitimu udereva wa bodaboda mabpo vijana zaidi ya 360 kutoka wilaya ya muleba wamefuzu mafunzo ya udereva wa boda boda ambayo yalidhaminiwa na mbunge wa jimbo hilo Profesa anna Tibaijuka .(Picha na Adam Mzee)




BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

KATIBU MKUU WA CCM KOMREDI KINANA AHANI MSIBA WA MAREHEMU MHE.SAMUEL LUANGISA MJINI BUKOBA LEO‏

Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya Marehemu Jaji Mstaafu Samuel Luangisa nyumbani kwake kwa marehemu Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.Marehemu Luangisa ni miongoni  mwa Waasisi wa Taifa na katika vipindi tofauti tofauti alikuwa mkuu wa Mkoa wa Ziwa Magharibi (Kagera),Mbunge na Meya wa Manispaa ya Bukoba pamoja na nyadhifa nyingine.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiweka shada la maua kwenye kaburi la Marehemu Jaji Mstaafu Samuel Luangisa mapema leo asubuhi nyumbani kwake kwa Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.
Katibu Mkuu Ndugu Kinana na baadhi ya maofisa wa chama na ndugu na jamaa wa marehemu wakishiriki sala ya pamoja na kumuombea marehemu Mzee Samuel Luangisa nyumbani kwake Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera
Katibu Mkuu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitia saini kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maombolezo ya Marehemu Mh. Samuel Luangisa nyumbani kwake mapema leo asubuhi,Kitendagulo,mjini Bukoba mkoani Kagera.

PICHA NA MICHUZI JR-BUKOBA.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa