Home » » Madereva wakorofi waonywa

Madereva wakorofi waonywa

MKUU wa Mkoa wa Kagera, Kanali Mstaafu, Fabian Massawe, amewaonya madereva wa vyombo vya moto mkoani hapa kujiepusha na uvunjaji wa sheria za barabarani.
Amesema madereva lazima watii sheria za barabarani bila shuruti, na kwamba serikali haitasita kuwakamata wanaovunja sheria.
Kanali Massawe alitoa onyo hilo juzi wakati wa sherehe za maadhimisho ya wiki ya usalama barabarani, ambayo kimkoa ilifanyika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.
Massawe ambaye alikuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo, ambayo kitaifa yalifanyika jijijni Mwanza, alisema lengo la kuwepo maadhimisho hayo ni kuielimisha jamii juu ya matumizi ya barabara na sheria za nchi.
“Ajali za barabarani zinaathiri sana maisha ya wananchi wetu. Kwa hiyo natoa onyo kwa madereva wote kuzingatia sheria,” alisema.
Alisema jamii kutojua vizuri sheria zikiwemo za barabarani, kimekuwa chanzo kikubwa cha ukiukwaji wa sheria na kutokea ajali ambazo nyingi husababisha vifo.
Aliwaomba watembea kwa miguu na waendesha vyombo vya moto kuwa makini na kuzingatia sheria za barabarani, kani itasaidia kupunguza ajali.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa