Home » » ASHA BARAKA AMUONYA DIAMOND KWA UNGA

ASHA BARAKA AMUONYA DIAMOND KWA UNGA


Mkurungezi wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ Asha Baraka.

Na Laurent Samatta
Mkurungezi wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ Asha Baraka amemuonya msanii anayefanya vizuri kwenye muziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kutojaribu kujihusisha na utumiaji wa madawa ya kulevya na kusema akijaribu atapotea.

Akizungumza na Ijumaa hivi karubini, Asha Baraka ‘Iron Lady’ alisema Diamond anaweza kufanya vizuri kwa miaka mingi inayokuja lakini akijaribu kutumia dawa hizo ataishia pabaya.

“Tumeona wasanii wengi wa Tanzania ambao awali walikuwa wanafanya vizuri lakini baada ya kujaa sifa na kukutana na marafiki wengi pamoja na makundi wakazama kwenye dawa za kulevya na sasa wanatapatapa na kubaki kulaumu wakati wenyewe wamejiharibia,” alisema Iron Lady.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Wasani ambao awali walikuwa wakifanya vizuri kimuziki lakini baadaye ‘wakadrop’ baada ya kujiingiza kwenye matumizi ya unga ni pamoja na Chid Benzi, Ray C, Q Chiller, Lord Eyez, Msafiri Diof na wengine ambao sasa wameshafariki.
Chanzo: Vijimambo blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa