Home » » NIKO FITI KWA AJILI YA KUWATUMIKIA WATANZANIA, NIPENI URAIS NITAFANYA KAZI USIKU NA MCHANA‏

NIKO FITI KWA AJILI YA KUWATUMIKIA WATANZANIA, NIPENI URAIS NITAFANYA KAZI USIKU NA MCHANA‏

1
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akitoa mpya jukwaani kwa kupiga Push Up kama kumi hivi ili kuwadhihirishia wananchi wa Mjini Karagwe mkoani Kagera kuwa yuko fiti kiafya ili kuwatumikia watanzania mara atakapochaguliwa na watanzania kuiongoza na kuwatumikia watanzania ifikapo Oktoba 25 mwaka huu katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani akisema kwamba kazi ya kuwatumikia watanzania siyo rahisi ni muhimu kuwa na afya njema ili kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na niko tayari kufanya kazi usiku na mchana.
Akizungumza katika mkutano huo ameongeza kuwa atahakikisha anapunguza kwa kiwango kikubwa kodi zinazotozwa kwa wakulima wa zao la kahawa ili bei ya zao hilo iweze kupanda na wakulima hao kufaidika na zao hilo badala ya kuhangaika kupeleka nchini Uganda ambako bei yake iko juu kuliko nchini Tanzania.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-NGARA)
2
1
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akihutubia wananchi wa jimbo la Kyerwa katika mkutano wa kampeni uliofanyika jimboni humo.
2
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akifurahia jambo katika mkutano huo.
3
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akisisitiza jambo wakati akizungumza na wananchi wa Kyerwa mkoani Kagera.
4
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Kyerwa Ndugu Innocent Sebba Bilakwate.
5
Umati wa wananchi ukiwa katika mkutano wa kampeni wa Dk John Pombe Magufuli uliofanyika mjini Ngara
7 9 10
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Ngara Ndugu Alex Raphael Gashaza aliyeshika ilani ya Uchaguzi.
11
Mgombea ubunge viti maalum vijana mkoa wa Kagera Bi. Halima Bulembo akizungumza katika mkutano wa kampeni uliofanyika mjini Ngara leo jioni.
12
mgombea ubunge wa jimbo la Ngara Ndugu Alex Raphael Gashaza akiomba kura kwa wana Ngara katika kutano huo.
15
Baadhi ya vijana wakiwa wamekaa katika milingoti ya magoli ya uwanja wa mpira wa shule ya sekondari ya Rumanyika wilayani Kyerwa.
16 17
Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Kagera Bw. Hamim akizungumza na wananchi katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo la Kyerwa kwenye uwanja wa shule ya sekondari ya Rumanyika.
18
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Karagwe Ndugu Innoncet Bashungwa.
20
Baadhi ya wananchi wakiwa na mabaongo yenye picha ya Dk John Pombe Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika mji wa Bunazi wilaya ya Misenyi.
21
Sheikh mkuu wa wilaya ya Mizenyi Abdulkadir Bulembo akifanya sala mara baada ya Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli kuhutubia mkutano wa kampeni mjini Bunazi wilayani Misenyi.
22
Baadhi ya wananchi wakiwa katika mkutano huo mjini Bunazi.
24
Hii ni kampeni si urembo kichwani.
25
Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli akimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Nkenge Balozi Deodoras Kamala mjini Bunazi.
26
Msafara wa Mgombea Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Dk. John Pombe Magufuli ukiwasili katika eneo la mkutano mjini Bunazi wilayani Misenyi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa