Home » » TRA KUPAMBANA NA WAFANYABIASHARA ZA MAGENDO

TRA KUPAMBANA NA WAFANYABIASHARA ZA MAGENDO


 Kamishna wa Mamlaka ya mapato nchini(TRA)Charles Kichere(wa pili kutoka kushoto)akiongea na waandishi wa habari kwenye ofisi za mamlaka hiyo Mkoa wa Kagera(hawapo pichani)juu ya ziara yake ya kikazi katika Wilaya zote za Mkoa wa Kagera
Mkurugenzi wa huduma ya elimu kwa mlipa kodi Richard Kayombo(wa kwanza kushoto)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani)

Na Editha karlo wa blog ya jamii,Kagera

MAMLAKA ya mapato(TRA)itaendelea kudhibiti na kupambana na wafanyabiashara wasio waaminifu wanaofanya biashara za magendo katika vituo mbalimbali na maeneo ya mipakani.

Kamishina mkuu wa mamlaka ya mapato nchini (TRA) ,Charles Kichere ameyasema hayo kwenye ofisi za mamlaka hiyo Mkoani Kagera wakati akiongea na waandishi wa habari juu ya ziara yake ya kikazi aliyoifanya katika Wilaya zote za Mkoani humo.

Alisema TRA itazidi kupambana na kuwabana wafanyabiashara wote wanaopitisha mizigo yao kwa njia ambazo siyo za halali na kufanya serekali ikose mapato.Aliwataka wafanyabiashara wanaotumia mpaka wa mtukula kupitisha mizigo yao kuingia nchini Tanzania na kwenda nchi ya jirani ya Uganda kupitisha mizigo yao kwani huduma sasa hivi kituoni hapo zinapatika kwa haraka.

"Sasa hivi tutaziba mianya yote inayosababisha upotevu wa mapato hususani katika mipaka yetu,nina waomba wafanyabiashara wote watumie njia zilizo halali kupitisha mizigo yao watakapo kamatwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kutaifishwa mizigo yao na kufikishwa katika vyombo vya dola"alisema.Alisema mamlaka haitavumilia vitendo vyovyote vya rushwa bali wataendelea kuwashughulikia mafisadi bila ya uogo wowote.Alisema tetemeko la ardhi lililotokea Mkoani Kagera miaka ya hivi karibuni liliathiri ukusanyaji wa kodi za majengo kwani nyumba nyingi ziliathiriwa na tetemeko.

"Nimeona wakazi wa Kagera ni walipa kodi wazuri,maeneo niliyotembelea nimeona wanatumia mashine za kieletroniki za kodi(EFD's)wanapouuza au kutoa huduma"alisema Kamishna.Alisema mamlaka haitawavumilia wafanyabiashara wanaoikosesha mapato serekali kwa kuuza au kutoa huduma bila ya risti za EFD's kwa makusudi.Mkurugenzi wa huduma ya elimu kwa mlipa kodi Richard Kayombo amewataka wananchi kuwa mabalozi wa ukusanyaji wa mapato kwa kutimiza wajibu wao wa kudai risti wanaponunua bidhaa au kupatiwa huduma mbalimbali.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa