Home » » Madiwani wataka mgodi uongeze mrabaha

Madiwani wataka mgodi uongeze mrabaha


Na Ali Lityawi, Biharamulo
MADIWANI wa Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo, mkoani Kagera wamemtaka mwekezaji wa mgodi wa dhahabu wa Tulawaka aongeze malipo ya mrabaha kwa madai kuwa sh milioni 300 kwa mwaka zinazotolewa kaziendani na uzalishaji wanaoufanya.
Akizungumza kwenye kikao cha baraza la madiwani, diwani wa Nyabusozi, Musure Bitanabona, alimtaka mwekezaji huyo kuongeza fedha za mrabaha zinazolipwa kwa mwaka kwa halmashauri kwa kuwa fedha hiyo hakiendani na faida kubwa anayoipata.
“Mheshimiwa mwenyekiti siungani mkono malipo ya mrabaha yanayolipwa na mgodi wa Tulawaka…hawa watu wamekuwa wakitupatia kiasi kidogo sana cha fedha ukilinganisha na uzalishaji wanaoufanya, ziara tuliyofanya mgodini imetufumbua mengi, tumeshuhudia kazi zinavyofanyika mgodini hapo.
‘Kwanza mazingira yetu wameyaharibu sana na tuliona mashimo marefu ambayo hata huwezi kufika kwa macho…hii inaonyesha wazi jinsi mwekezaji huyo anavyonufaika na rasilimali zetu huku sisi tukiendelea kutaabika,” alisema Bitanabona.
Hoja hiyo iliungwa mkono na madiwani wengie na kutaka mwekezaji huyo kuongeza fedha za mrabaha na kufuikia sh bilioni moja, ili iwe rahisi kwa halmashauri hiyo kupeleka maendeleo kwa wananchi wake.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa