Home » » Radi yaua sita Kagera

Radi yaua sita Kagera


Na Mbeki Mbeki, Bukoba


WATU sita wamefariki dunia kwa kupigwa na radi, watatu wakiwa wa familia moja katika Kata ya Kibingo, Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Phillip Kalangi, aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Methodia Kaledunia (35), Bateganya Kamashana (miezi 10) na Kamugisha Kamashara (2).
Wengine waliokufa ni Kazungu Emmanuel (15), mwanafunzi wa darasa sita Shule ya Msingi Kihinda, Dawson Aaron (16) mwanafunzi wa darasa la saba katika Shule ya Msingi Kihinda na Revelian Wilison (4).
Alisema tukio hilo lilitokea Juni 8, majira ya jioni katika Kijiji cha Kihinda, wilayani Kyerwa na kwamba watu hao walikuwa wamejikinga na mvua kwa jirani yao.
Aidha, alisema katika tukio hilo pia mbuzi watano walikufa kwa kupigwa na radi, nyumba moja na baadhi ya mashamba yaliharibiwa vibaya.
Mtendaji wa kijiji hicho, Jofrey Milambwe, alisema watu watatu wa familia moja wamezikwa katika kaburi moja kutokana na mwili yao kuharibika vibaya.

Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa