Home » » Wazee watakiwa kutojihusisha na siasa

Wazee watakiwa kutojihusisha na siasa


na Antidius Kalunde, Bukoba
WAZEE wameshauriwa kutojihusisha na siasa na badala yake watafute mbinu za kukabiliana na hali ngumu ya maisha, ili kuepuka kuwa ombaomba katika maisha yao ya kila siku.
Ushauri huo ulitolewa na Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Bukoba, Mrisho Issa kwa niaba ya mkurugenzi wa manispaa hiyo wakati wa kufungua tawi la Saidia Jamii ya Wazee Kagera (SAJAWAKA) tawi la Kata ya Kahororo katika manispaa hiyo ambalo limeanzishwa kwa ajili ya kusaidia wazee.
Alisema wazee wanapofungua vikundi kama hicho wanapaswa wajue malengo yake na wala wasijihusishe na siasa, kwani wakati wa kushabikia masuala ya siasa yawe nje ya vikundi hivyo.
Aliongeza kuwa vipo vikundi vingi vinaanzishwa lakini malengo ambayo yamekuwa yamekusudiwa hayafanyiwi kazi na badala yake wanashabikia mambo ya kisiasa.
Katika hatua nyingine, alisema pamoja na kufungua tawi la wazee bado kuna changamoto kwa wazee kutopata huduma ya afya bure hasa wale waliotimiza miaka 60 na kuendelea kama sera ya wizara inavyosema.
Nae Mwenyekiti wa tawi la Saidia jamii ya wazee Kagera tawi la Kata ya Kahororo, Silivandi Muyoza alisema kikundi hicho hakikuanzishwa kwa lengo la siasa na badala yake ni kwa ajili ya kusaidia wazee kimaendeleo kwa kubuni miradi mbalimbali.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa