Home » » Jambazi auawa akutwa na silaha kali za kivita, mabomu 3, bunduki 3 AK 47na risasi 246

Jambazi auawa akutwa na silaha kali za kivita, mabomu 3, bunduki 3 AK 47na risasi 246



Na Theonestina Juma, Bukoba

JESHI la polisi Mkoani Kagera limefanikiwa kuua jambazi mmoja na kukutwa na silaha kali za kivita zikiwemo bunduki tatu, risasi 246 mabomu matatu ya kurushwa kwa mkono wakiwa katika harakati za kutaka kuvamia mgodi wa Tulawaka wilani Biharamulo.

Hayo yamebainishwa na Kamanda wa polisi Mkoani Kagera, Philip Kalangi wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mapema leo asubuhi na kwamba tukio hilo lilitokea Juni 9,m mwaka huu saa 10.30 alafajiri Mavota Tulawaka wilayani humo.

Kamanda Kalangi alisema jambazi huyo aliuawa baada ya polisi kupambana na kundi la majambazi wasiojulikana idadi kwa dakika kadhaa,  ambao walizidiwa nguvu na mmoja kuuawa na wengine kukimbilia kusikojulikana.

Alisema baada ya jambazi huyo kuuawa alipopekuliwa alikutwa na silaha hizo, zikiwemo bunduki tatu aina ya AK 47 mbili zikiwa na namba UC 55231990,
UC 16081998 na pamoja  na bunduki aina ya Short gun mashine  (SMG) yenye namba 56128033262 ambapo mbili zikikuwemo kwenye mfuko wa kiroba ambayo alikuwa akiitumia katika kujihami katika tukio hilo.

Alisema mbali na kukutwa na silaha hizo pia alikutwa na sare pea mbili ambazo zinafanana na za Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) buti jozi moja koti ya mvua ambazo zilikuwwa zimefungiwa bunduki mbili na magazine saba zilizokuwa na risasi.

Alisema mwili wa jambo huyo umehifadhiwa katika hospitali Teule ya Wilaya ya Biharamulo  ambapo msako unaendelea wa kuwatafuta majambazi wengine waliokimbia kusikojulikana.

Chanzo-Rorya Kwetu Blog

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa