Home » » DC AAMURU MWALIMU ACHUNGUZWE

DC AAMURU MWALIMU ACHUNGUZWE


na Ashura Jumapili, Bukoba
MKUU wa Wilaya ya Ngara, Constantine Kanyasu, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Ngara kufanya uchunguzi wa siku 14, ili kubaini tuhuma mbalimbali zinazomkabili Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kabanga, Enock Ntakisigaye, ikiwemo kutumia majina hewa ya walimu kujipatia fedha pamoja na matumizi mabaya ya fedha na mali za shule.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, mkuu huyo wa wilaya (DC), alisema ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa za kuwepo mgomo baridi wa kufanya kazi kutoka kwa walimu wa shule hiyo kutokana na tuhuma kadhaa ambazo walikuwa wamelalamika kwa muda mrefu bila kufanyiwa kazi.
Alisema kutokana na tuhuma hizo ameamua kumuagiza mkurugenzi kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.
Aliongeza katika kipindi hicho, mkuu wa shule, Enock Ntakisigaye, makamu wa shule, Daud Michael, na Mhasibu, Kalenzo Majanja, watakuwa nje ya ofisi kupisha uchunguzi.
Chanzo: Tanzania Daima
 DC AAMURU MWALIMU ACHUNGUZWE
na Ashura Jumapili, Bukoba
MKUU wa Wilaya ya Ngara, Constantine Kanyasu, amemuagiza Mkurugenzi wa Halmshauri ya Ngara kufanya uchunguzi wa siku 14, ili kubaini tuhuma mbalimbali zinazomkabili Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Kabanga, Enock Ntakisigaye, ikiwemo kutumia majina hewa ya walimu kujipatia fedha pamoja na matumizi mabaya ya fedha na mali za shule.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, mkuu huyo wa wilaya (DC), alisema ametoa agizo hilo baada ya kupokea taarifa za kuwepo mgomo baridi wa kufanya kazi kutoka kwa walimu wa shule hiyo kutokana na tuhuma kadhaa ambazo walikuwa wamelalamika kwa muda mrefu bila kufanyiwa kazi.
Alisema kutokana na tuhuma hizo ameamua kumuagiza mkurugenzi kufanya uchunguzi wa kina ili kubaini ukweli wa tuhuma hizo kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa.
Aliongeza katika kipindi hicho, mkuu wa shule, Enock Ntakisigaye, makamu wa shule, Daud Michael, na Mhasibu, Kalenzo Majanja, watakuwa nje ya ofisi kupisha uchunguzi.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa