Home » » Njaa yatishia Karagwe

Njaa yatishia Karagwe


na Mbeki Mbeki
VIJIJI 102 vya Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera viko hatarini kukumbwa na njaa kufuatia ugonjwa wa mnyauko kuangamiza zao la ndizi.
Tahadhari hiyo imetolewa jana na mtaalamu wa kilimo wa Wilaya ya Bukoba, Mugenzi Byabachwezi, wakati akitoa mada ya uboreshaji wa hali ya chakula duniani, na kudai kuwa wilaya hiyo na ile mpya ya Kyerwa zitakumbwa na baa hilo.
Alisema kuwa zaidi ya migomba 30,000 tayari imeshambuliwa na migomba 26,000 imefyekwa katika harakati ya kudhibiti ugonjwa hao hatari.
Alisema kuwa ugonjwa huo umeenea kwa kasi zaidi katika vijiji vilivyo mpakani na nchi ya Uganda ambako ugonjwa huo ndiko ulikotokea, kutokana na wafanyabiashara wengi wanaotoka huko na kuingia wilayani humo kwa ajili ya kununua ndizi na mara nyingine mashina ya migomba.
Aliongeza kuwa mbali na kuenea kwa njia ya upepo, matumizi ya mapanga wanayotumia kukatia migomba, hivyo akataka kusitishwa kwa matumizi ya zana hizo kabla ya kuzipitisha kwenye moto.
Mtaalamu huyo alisema namna pekee ya kukabiliana na janga hilo ni kwa wananchi kulima mazao mengine ya chakula kuliko kutegemea misaada kutoka nje
Chanzo: Tanzania Daima


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa