Home » » WALIMU WAFUNDWA JUU YA MIKOPO

WALIMU WAFUNDWA JUU YA MIKOPO


na Mbeki Mbeki, Karagwe
WALIMU wilayani Karagwe, Kagera wametakiwa kujenga utamaduni wa kuchukua mikopo inayoendana na uwezo wao kiuchumi na mishahara yao.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wilayani hapa Velenan Vedasto, alipozungumza na waandishi wa habari juu ya changamoto mbalimbali za kiuchumi zinazowakabili walimu.
Vedasto alisema walimu wanapaswa kuchukua mikopo inayoendana na uwezo wao wa mishahara, ili iweze kuleta tija katika familia zao.
Alisema utafiti uliofanywa na ofisi yake hivi karibuni ulibaini walimu 23 hawana mishahara kabisa na wengine 65 wanapokea mishahara chini ya sh 50,000 kwa mwezi.
“ Kwa kweli hii ni hatari kwa familia za walimu, mwisho wa mwezi hana mshahara…mwalimu wa aina hii hata akaingia darasani kufundisha hata mwanafunzi anamuelewa?” alihoji Vedasto.
Alisema baadhi ya walimu wamekuwa wanakopa mikopo mikubwa katika taasisi za fedha ambayo haiendani na vitega uchumi vyao, matokeo yake kushindwa kurejesha mikopo kwa wakati na wakati mwingine kuziathiri familia zao.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa