Home » » KAGERA WAHIMIZWA KUJIUNGA NSSF

KAGERA WAHIMIZWA KUJIUNGA NSSF

WANANCHI mkoani Kagera, wametakiwa kujiunga na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), ili waweze kupata mafao bora ikiwemo bima ya afya bure kwa familia.
Wito huo ulitolewa mjini hapa jana na Meneja wa Mafao ya Matibabu wa NSSF, Dk. Ally Mtulia, alipokuwa akisoma taarifa ya utakelezaji mkoani hapa katika siku ya zoezi la upimaji wa afya bure kwa Kanda ya Ziwa.
Dk. Mtula alisema shirika hilo litaendelea kuwahimiza wananchi kujiunga nalo, kwani kuna mafao mengi wanaweza kunufaika nayo na pia wanaweza kujipatia mikopo hasa wajasiriamali wadogo, ushirika wa bodaboda, wakulima kupitia vyama vya akiba na mikopo.
Alisema  mbali na kujiunga na NSSF, amewaomba wananchi  hao kujijengea tabia ya kupima afya zao, ili kujiwekea mfumo bora wa maisha ikiwa ni pamoja na kuepuka magonjwa sugu.
Zoezi la kila mwananchi kupima afya lilianzia mkoani Mara, Shinyanga, Geita ambako watu wengi walijitokeza kupima afya zao.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa