Home » » 'PAMBANENI NA UVUVI HARMU'

'PAMBANENI NA UVUVI HARMU'

WANANCHI wa Wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, wametakiwa kutumia elimu wanayopewa na maofisa uvuvi kupambana na kutokomeza uvuvi haramu, ili kuokoa kuangamia kwa Ziwa Victoria.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Ofisa Uvuvi Wilaya ya Muleba, Siymphorian Ngaiza, alipozungumza na Tanzania Daima ofisini kwake, kutokana na kuongezeka kwa vitendo vya uvuvi haramu katika ziwa hilo.
“Jamii ina wajibu mkubwa wa kudhibiti vitendo vya uvuvi haramu kwa vile wao ndio wanaoishi na wavuvi wenye tabia kama hizo,” alisema.
Alisema kuwa aina ya uvuvi haramu ulioshamiri katika Wilaya hiyo ni ule wa kutumia nyavu zisizoruhusiwa ambazo ziko chini ya kiwango na zinazonasa samaki wadogo.
Aliwataka wavuvi kuzingatia sheria zilizopo ikiwa ni pamoja na kulipia ushuru wa usafirishaji wa samaki ili kuepuka usumbufu unaojitokeza wa kukamatwa.
Pia aliwashauri wakazi wa visiwani humo kuanzisha ulinzi shirikishi, ili kuwabaini wageni wanaojihusisha na vitendo vya wizi wa injini na zana nyingine za uvuvi na kuwafikisha katika kituo cha polisi.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa