Home » » WATAHADHARISHWA KUEPUKA MAGONJWA

WATAHADHARISHWA KUEPUKA MAGONJWA

WAKAZI wa Wilaya ya Muleba mkoani Kagera, wametakiwa kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa wa malaria ili kupunguza idadi ya vifo vya watoto na wajawazito.
Kauli hiyo imetolewa  jana na Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya,  Leontine Rwamulaza wakati  akihojiwa na Tanzania Daima  ofisini kwake kuhusiana na mlipuko wa magonjwa wilayani kwake.
Rwamulaza alisema wilaya hiyo inaongoza kwa ugonjwa huo katika Mkoa wa Kagera, na hivyo akawataka wananchi kuzingatia sheria na masharti ambayo wanakuwa wanapewa na wataalamu wanazunguka  katika vijiji.
Alisema wamechukua hatua za kupambana na ugonjwa huo kwa kuanzisha utaratibu wa kutembelea vijiji kupima kila mtu na ambae anabainika kuwa na ugonjwa huo hupewa dawa  ikiwa ni pamoja na kutakiwa kuweka mazingira safi ili kuondoa mazalia ya mbu.
“Wilaya yetu ni kati ya wilaya tisa hapa nchini zinazoongoza kwa ugonjwa huu, na hii inatokana na kuwa na mito inayoaminika kuwa na mbu wengi na ambayo pia wananchi wanaishi karibu nayo,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa