Home » » WAFANYABIASHARA WATAKA UMOJA EA

WAFANYABIASHARA WATAKA UMOJA EA

Wafanyabiashara wataka umoja EABAADHI ya wafanyabiashara walioshiriki Maonyesho ya Sabasaba katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kutoka nchini Kenya, wameitaka Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EA) kuondoa vikwazo mipakani kwa nia ya kuendeleza fursa za masoko na maendeleo.
Mmoja wa wafanyabiashara hao, Elizabert Ogake, ameliambia Tanzania Daima Jumapili kuwa hupata usumbufu mpakani wanaposafisha bidhaa zao na kutozwa fedha nyingi kinyume na sheria.
Alibainisha kuwa hupata misukosuko ya kutozwa ushuru wa bidhaa kutoka Idara ya Uhamiaji ya Uganda.
Alisema uwepo wa Maonyesho ya Sabasaba yanayofanyika kila mwaka, husaidia kukutanisha wafanyabiashara wa nchi hizo ambao hupeana mbinu za kukuza uchumi wa nchi zao.
Mkurugenzi wa Shirika la Kagera Agricultural Industrial Development & Promotion (KAIDEP), Philemon Kamazima, waliodhamini maonyesho hayo, alisema kulikuwa na mwitikio mzuri mwaka huu tofauti na miaka mingine.
Alisema maonyesho ya mwaka huu yalikuwa na washiriki 255  kutoka ndani na nje ya nchi ambapo wengi wao wametoka katika makampuni na taasisi mbalimbali za uzalishaji mali kutoka nchi za Uganda, Kenya na Rwanda.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa