Home » » RC MASSAWE AIPIGANIA BUWASA

RC MASSAWE AIPIGANIA BUWASA

MKUU wa Mkoa wa Kagera (RC), Kanali mstaafu Fabian Massawe, amezicharukia taasisi, makampuni na watu binafsi wanaoshindwa kulipa bili za maji katika Mamlaka ya Majisafi na Majitaka ya Manispaa ya Bukoba mkoani hapa (BUWASA).
Aliyasema hayo juzi wakati akizungumza kwenye  uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Maji, yaliyofanyika katika uwanja wa ofisi ya Kata ya Kibeta, Manispaa ya Bukoba.
Massawe aliitaka mamlaka hiyo kusitisha huduma ya maji pindi mteja wake anaposhindwa kulipa bili za maji ili kuokoa hasara inayoweza kuikumba mamlaka hiyo
Chanzo:Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa