Home » » ‘Wazazi pelekeni watoto vyuo vya ufundi’

‘Wazazi pelekeni watoto vyuo vya ufundi’

WAZAZI na walezi wametakiwa kuwapeleka watoto wao waliohitimu kidato cha nne katika vyuo mbalimbali vikiwemo  vya ufundi na utalii, ili kuwaongezea utaalamu zaidi.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Diwani  wa Viti Maalumu, Joyce Mirembe Aenda, alipozungumza na waandishi wa habari mjini Kayanga.
“Kushindwa kuendelea na kidato cha tano si kwamba mwanao hana akili au uwezo wa kujiendeleza, ondoa fikra  hizo, pelekeni watoto shule,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa