Home » » Diwani ataka serikali iongeze walimu

Diwani ataka serikali iongeze walimu

BARAZA la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Muleba, Kagera, limeiomba serikali kujizatiti zaidi kuzalisha walimu wengi hapa nchini ili kukuza sekta hiyo muhimu.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na baadhi ya madiwani wa halmashauri hiyo, walipokuwa wakizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani.
Walisema upo umuhimu kwa serikali kuweka mkazo zaidi wa kuzalisha walimu wengi wakiwemo wa masomo ya sayansi na hisabati, na kuleta walimu wa kujitolea kutoka nje ya nchi.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa