Home » » Walimu Karagwe waomba mafunzo JKT

Walimu Karagwe waomba mafunzo JKT

WALIMU wa shule za msingi na sekondari wilayani Karagwe, wameitaka serikali kurudisha mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria, ili kuwajengea ukakamavu katika maeneo yao ya kazi.
Wakizungumza katika mkutano mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) jana, uliowajumuisha walimu wa Wilaya ya Karagwe na Kyerwa, walisema walimu waliopitia mafunzo ya JKT na ambao hawajapitia wanaonekana wako tofauti kiukakamavu na katika utendaji kazi wao.
“Serikali itupeleke jeshini tukapate ukakamavu. Tuliwaona walimu waliopita jeshini walikuja na vitu vingi vya kuiga, nyimbo za hamasa za mchakamchaka, gwaride, michezo mbalimbali,” alisema.
Chanzo;Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa