Home » » WALIMU WANAOHUDHURIA MIKUTANO YA SIASA YA WAPINZANIA WAWAJIBISHWA

WALIMU WANAOHUDHURIA MIKUTANO YA SIASA YA WAPINZANIA WAWAJIBISHWA

Chama cha Walimu (CWT) Manispaa ya Bukoba Mkoa Kagera  kimesema kama mwalimu atawajibishwa kushiriki kuhudhuria mikutano ya vyama vya upinzani awajibishwe pia kuhudhuria mikutano ya Chama Cha Mapinduzi.wakati wa uchaguzi mkuu wa Serikali za Mtaa.

Hayo yametolewa na Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu (CWT) Mkoa Kagera Bw.Dauda Bilikesi wakati wa mkutano mkuu wa chama hicho uliofanyika (leo ijumaa) kwenye ukumbi wa Red Cros ulioko Manispaa ya Bukoba.

Bw.Bilikesi amesema CWT itahakikisha haki inatendeka kwa vyama vyote kwani vyama hivyo vya siasa ni vizawa na hivyo mwalimu ana haki ya kusikiliza hali mradi asishiriki kuvaa sare,kupiga kampeini au kuchochea wapigakura waunge mkono chama kimoja.

Mwenyekiti Bilikesi amesema wapo baadhi ya viongozi wa siasa wameanza kutishia baadhi ya walimu  wawajibishwe baada ya kwenda kusikiliza mikutano ya viongozi wa vyama vya upinzani wakidai wasipowajibishwa wahamishwe.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Walimu  (CWT) Manispaa ya Bukoba  Bw.Laulean Kashaija amewaasa walimu hasa wafundishao shule za sekondari wasiwe wachochezi wa kuwaongoza wanafunzi wamchague kiongozi yupi kati ya wagombea.

Bw.Kashija amesema walimu wa sekondari wanatakiwa kufundisha somo la Uraia kama mwongozo unavyoelekeza kama masomo ya kawaida.

Mkutano mkuu huo ulihudhuliwa na viongozi ambao ni walimu wawakilishi kutoka sehemu mbali mbali za kazi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa