Home » » Mgeja atamba CCM ipo imara hakuna wa kuiyumbisha

Mgeja atamba CCM ipo imara hakuna wa kuiyumbisha

Baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Byantanzi, wilayani Muleba, wamemuomba Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Anna Tibaijuka,  kushughulikia  mgogoro wa ardhi inayodaiwa kuuzwa kwa mwekezaji.
Wakizungumza na gazeti hili juzi katika kijiji hicho, wananchi hao walisema uongozi wa  wilaya, umewapa muda wa miezi sita kuhama katika eneo linalodaiwa kumilikiwa na mwekezaji.
Walisema hata hivyo amri hiyo imetolewa  bila wao kupewa maeneo mbadala ya kuendesha maisha yao.
Walielezea kushangazwa kwao juu ya taarifa za kuuzwa kwa eneo hilo kwa mwekezaji, wakati  uongozi wa kijiji ukiwa hauna taarifa.
Mmoja wa wananchi hao, Faston Benson, alisema wananchi katika kijiji hicho, wamekumbwa na hofu baada ya kuelezwa kuwa wanatakiwa kuhama ili kumpisha mwekezaji.
Diwani wao, Khalid Hussein (Chadema) alielezea kushangazwa kwake juu ya  amri iliyotolewa na uongozi wa wilaya hiyo ikiwataka wananchi, kuhama katika eneo hilo.
Alisema inashangaza kuwa viongozi waliotoa amri hiyo, hawakuwahi kwenda katika kijiji hicho  na kuwasikiliza wananachi.
Mwenyekiti wa Kitongozi cha Ntungamo, katika kijiji hicho, Desdery Hurubano alisema zaidi ya kaya 300 katika eneo hilo zinaishi kwa hofu kutokana na vitisho vya kuhamishwa.
Aliwasihi uongozi wa wilaya kwenda  katika kijiji hicho ili kusikiliza malalamiko ya wananchi badala ya kuwapa vitisho vya kutaka wampishe mwekezaji.
Hurubano alisema jambo hilo halikubaliki na kwamba ni vizuri viongozi waka wazi  kwa wananchi wa kijiji hicho.
Kiongozi huyo wa kitongoji alisema inashangaza na kusikitisha kuona wananchi walioishi katika eneo kwa muda mrefu, waamriwa kuhama bila kushirikishwa.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa