Home » » ‘Wanawake, watoto tambueni haki zenu’

‘Wanawake, watoto tambueni haki zenu’

WANAWAKE na watoto wametakiwa kuzitambua haki zao za kimsingi katika jamii ili kuepukana na vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia vinavyokithiri wilayani Karagwe.
Mkurugenzi Mtendaji wa asasi isiyo ya kiserikali ya Women’s and Men’s Development Association (WOMEDA) iliyopo mjini Kayanga, wilayani hapa, Juma Masasi, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Alisema wanawake wilayani humo wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili ikiwemo ukatili wa kingono, ukatili wa kimwili na ukatili wa kisaikolojia.
Masasi alisema shirika lake limeweza kupokea kesi mbalimbali za aina hiyo zikiwemo za ndoa, talaka, mikataba ya ajira, za madai na mirathi.
Alisema shirika lake kwa kuungana na mashirika mengine kama Chama cha Wanahabari Wanawake (Tamwa), madawati ya kijinsia watahakikisha wanapambana na vitendo vya kikatili bila woga.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa