Home » » Wakazi wakiri kula kinyesi bila kujua wilayani Karagwe

Wakazi wakiri kula kinyesi bila kujua wilayani Karagwe

Karagwe. Baadhi ya wananchi wa  Kijiji cha Kafunjo, Kata ya Kiruruma, wilayani Karagwe, mkoani Kagera, wamesema wamekuwa wanakula kinyesi bila kujua kutokana na kutokuwa na vyoo bora.
 Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara kijijini hapo  mwishoni mwa wiki iliyopita, baada ya kutembelewa na Ofisa wa Afya kutoka Ofisi ya Mganga Mkuu Wilaya ya Karagwe, kuwaelimisha jinsi ya ujenzi wa vyoo bora na matumizi yake.
Mmoja wa wakazi hao,  Renatus Kanyabuhura alisema kutokana na kutokuwa na vyoo bora, walikuwa wakila kinyesi kwa sababu walikuwa wakitoka chooni bila kunawa mikono na kuvuta sigara huku  wengine kula matunda.
“Kutokana na kutokuwa na vyoo bora, unakuta nzi wanaotoka chooni wanatua kwenye chakula na huku mlaji anaendelea, jambo linalojionyesha tunakula kinyesi,” alisema Kanyabuhura.
Naye Ofisa wa Afya, Moses Aligawesa alisema magonjwa mengi yanatokana na matumizi mabaya ya vyoo na kula kinyesi kwa njia tofauti.
Aligawesa alitaja magonjwa yanayotokana na kula kinyesi kuwa ni, kipindupindu, kuhara, kichocho, safura (minyoo) na kwamba,  magonjwa hayo yanaathiri kila mmoja kuanzia familia, kijiji, kata hadi taifa. Alisema choo bora ni shimo lenye urefu wa futi 12 na kuendelea, kinachosafishika, kuezekwa   bila kusahau kunawa mikono kwa kutumia maji na sabuni.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa