Home » » HUDUMA ZA UJUMBE MFUPI WA MANENO (SMS) ZAZUIWA MKOANI KAGERA

HUDUMA ZA UJUMBE MFUPI WA MANENO (SMS) ZAZUIWA MKOANI KAGERA


Kwa takriban mwezi sasa watumiaji wa simu za mkononi ya Vodacom hawawezi kutuma ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwenda kwa watumiaji wa airtel kwa sababu amabzo hazijawekwa wazi.

Mtandao wa Harakatinews umefanya mahojiano na wasemaji wa Vodacom kwa bukoba mjini amabo wamekiri kuwepo tatatizo hilo lakini wanaongeza kwamba tatizo haliko kwako (vodacom) bali lipo Airtel ambapo juhudu za kuwapata wasemaji wa Airtel bado zinaendelea.



"Hili tatizo ni kweli lipo,na wateja wetu wanalalamika sana lakini  halipo kwetu bali lipo kwa wenzetu ingawa linashuguhulikiwa' alisema afisa wa vodacom Bukoba mjini.

Uchuguzi wa mtandao huu umebaini kwamba watu wengi kwa kagera wanaotumia mtandao wa Vodacom   hawajui kwamba hawezi kutuma SMS kwa jamaa zao wanaotumia mtandao wa airtel.

Tutaendelea kuwajuza kama tatatizo limetatuliwa.

Chanzo: Harakatinews

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa