Home » » MSAKO WANASA BUNDUKI, VIROBA VYA KONYAGI

MSAKO WANASA BUNDUKI, VIROBA VYA KONYAGI

JESHI la Polisi mkoani Kagera limekamata bunduki moja ya kivita ikiwa imefukiwa ardhini pamoja na viroba bandia vya pombe aina ya konyagi katoni 20.
Hayo yalisemwa juzi na Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi.
Vitu hivyo vimekamatwa kufuatia msako mkali ulioanza kwa wiki moja kuanzia Agosti 18 mwaka huu katika maeneo ya nchi kavu na majini.
Kamanda Mwaibambe, alisema bunduki ya kivita iliyokamatwa ni aina ya Uzigan ambapo alibainisha kuwa ilipatikana baada ya raia wema kutoa taarifa. Alisema bunduki hiyo ilikutwa imefukiwa ardhini katika kisiwa cha Gozba wilayani Muleba.
Katika tukio la viroba bandia, Jeshi limemkamata Arbogastus Kamala (38) mfanyabiashara mkazi wa Kamizilente, Kata ya Hamgembe akiwa na katoni 20 za viroba bandia vya konyagi maeneo ya stendi kuu ya mabasi Bukoba.
Alisema katika hali ya kawaida, ni vigumu kwa mtu kutofautisha kiroba halali na bandia kwa sababu tofauti iliyopo ni ndogo sana huku akisema mhuri wa kiroba halali haufutiki na kwenye nembo ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeandikwa neno Konyagi na TBL (Kampuni ya Bia Tanzania) wakati bandia hakina maneno hayo na mhuri wake unafutika hata kwa kusugua kwa kidole.
Chanzo;Habari Leo 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa