Home » » IGP SIRRO ASISITIZA WELEDI KWA POLISI

IGP SIRRO ASISITIZA WELEDI KWA POLISI




Imeandikwa na Demetrius Njimbwi, Jeshi la Polisi


IGP Simon Sirro.
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro, amewataka askari wa jeshi hilo kufanya kazi kwa weledi na kwa kuzingatia sheria na taratibu zitakazosaidia kujenga taswira chanya hasa wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku.
Aliyasema hayo alipokutana na askari na maofisa wa mkoa wa Kagera, wakati akiwa kwenye mwendelezo wa ziara zake zenye lengo la kujitambulisha pamoja na kujua matatizo wanayokutana nayo wakati wakitekeleza majukumu yao.

Alisema kila askari analo jukumu mbele yake la kuhakikisha suala la uhalifu na wahalifu linadhibitiwa hususan kwa kuimarisha usalama wa raia na mali zao huku wakizingatia kuwa, mkoa huo unapakana na nchi za Uganda, Rwanda na Burundi.

Hata hivyo, katika ziara yake, IGP Sirro, amewahakikishia askari na maofisa kuwa, yupo tayari kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza na kuwataka askari kuongeza kasi ya kukabiliana na tishio la uhalifu na wahalifu ili kuifanya jamii kuishi kwa amani na utulivu.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa