Home » » MAWAZIRI 5 WATEMBELEA MPAKA WA TANZANIA, UGANDA

MAWAZIRI 5 WATEMBELEA MPAKA WA TANZANIA, UGANDA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi.
MAWAZIRI watano wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wametembelea mpaka wa Tanzania na Uganda ili kutatua changamoto zinazoukabili mpaka huo na kuuboresha.
Mawaziri hao ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi , William Lukuvi, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Selemani Jaffo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk Suzan Kolimba na Naibu Waziri wa Maji na Umwagiliaji , Mhandisi Isack Kamwelwe.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na wizara ya ardhi, miongoni mwa maeneo yaliyotembelewa na mawaziri hao ni eneo la mpaka ya Tanzania na Uganda kwa upande unapopita mto Kagera na eneo la kivuko cha mpaka wa Tanzania na Uganda kilichopo Mtukula mkoani Kagera.
Katika ziara hiyo, mawaziri hao walijionea hali halisi ya maisha ya wakazi wa mipakani na jinsi wanavyohusiana na wenzao wa nchi ya jirani ya Uganda, ambapo wamekuwa wakishirikiana na kuishi kwa amani katika shughuli zao za kila siku.
CHANZO HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa