Home » » KAGERA YAKUSANYA MIL35 KILA MWEZI SOKO LA SAMAKI

KAGERA YAKUSANYA MIL35 KILA MWEZI SOKO LA SAMAKI


SERIKALI mkoani Kagera inakusanya kati ya shilingi milioni 35 hadi 38 kila mwezi, kutokana na uuzwaji nje ya nchi samaki na dagaa waliokaushwa, wanaovuliwa katika ziwa Victoria

Afisa mfawidhi kitengo cha udhibiti ubora na usalama wa samaki na mazao yake katika mkoa wa Kagera, Monica Kishe amesema kuwa kwa mwezi Oktoba mwaka huu, ziliuzwa nje ya nchi tani 100 za samaki na tani kumi za dagaa wakavu na kuipatia serikali fedha za kigeni zaidi ya shilingi milioni 38.

Amezitaka halmashauri za wilaya ya Bukoba, Muleba na manispaa ya Bukoba, kushirikiana na wavuvi katika wilaya hizo kutunza mialo saba inayokarabatiwa na serikali kuu kwa gharama ya shilingi bilioni 28, ili kuongeza ubora na upatikanaji zaidi wa samaki.

Mialo iliyokarabatiwa ni Nyamukazi,  Igabilo, Rushara, Marehe, Kerebe, Iramba na Katembe, na kuwa gharama ya kila mwalo ni shilingi milioni 400.

Hata hivyo amesema pamoja na mapato hayo samaki katika ziwa Victoria wanaendelea kupungua kutokana na uvuvi haramu unaoendeshwa na baadhi ya wavuvi, ikiwamo kuvua kwa sumu, matumizi ya nyavu zisizoruhusiwa kisheria na vyandarua.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa