Home » » MBUNGE AWAPELEKA WAKULIMA 120 KUJIFUNZA UGANDA

MBUNGE AWAPELEKA WAKULIMA 120 KUJIFUNZA UGANDA

Mwandishi wetu, Kagera Yetu
Wakulima 120 kutoka Wilaya ya Bukoba Mkoa Kagera wamepata fursa ya kwenda kujifunza jinsi ya kupambana na ugonjwa wa mnyauko wa migomba huko Mbarara nchini Uganda.

Akizungumza na waandishi wa habari mjinji Bukoba Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bukoba vijijini Bw. Ahmed Kyobya amesema kila kijiji kimewakilishwa na mkulima mmoja ambao idadi yao ni 92 baada ya kurudi watakuwa walimu wa wakulima kwenye vijiji vyao.

Bw. Kyobya amesema katika msafara huo wamo Madiwani kumi kutoka Halmashauri ya wilaya Bukoba, Maafisa Kilimo wanne,Maafisa wawili kutoka chuo cha utafiti wa kilimo Maruku na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mh,Jasson Rweikiza.

Katibu wa Mbunge huyo amesema ziara hiyo ya siku tatu itaanza Jumanne (Septemba, 18 mwaka huu) kuelekea Mbarara Uganda ambako watapata fursa ya kuwatembelea wakulima mbalimbali na kuwaonyesha jinsi wanavyopambana na ugonjwa huo wa mnyauko.

Aidha safari hiyo imedhaminiwa na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Vijijini Mh.Jasson Rweikiza baada ya kuona ugonjwa huo unazidi kuongezeka Mkoani Kagera.
Blogzamikoa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa