Home » » WANANCHI WAVAMIA MAHABUSU, WAUA MTUHUMIWA

WANANCHI WAVAMIA MAHABUSU, WAUA MTUHUMIWA

na Ashura Jumapili, Bukoba
WANANCHI wamevamia mahabusu ya Mahakama ya Mwanzo ya Muhutwe, wilayani Muleba na kuvunja milango na kumtoa mtuhumiwa, Faustine Rweyemamu (60), mkazi wa Ndolange-Kamachumu na kisha kumpiga hadi kumuua baada ya kufanya jaribio la kutaka kumwiba mtoto kwa kumpeleka maeneo ya msituni.
Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mtendaji wa Kijiji cha Bisore, Dominic Damasenyi, alisema mahabusu huyo ameuawa na wananchi kwa kutuhumiwa kuiba mtoto mwenye umri wa miaka 15, aitwaye Zakhia  Hashimu.
Damasenyi alisema wananchi walimuona mwanaume huyo akiondoka na mtoto huyo wakiwa wamefuatana kwa karibu kutokea maeneo ya Muhutwe stendi kuelekea Muleba mjini.
Alisema baada ya wananchi kuona hivyo, walishituka na kuanza kumfuatilia na walipomkamata, askari walimpeleka katika mahabusu hiyo.
“Hali hiyo ilisababisha wananchi wenye hasira kuvamia selo hiyo na kisha kumtoa mtuhumiwa huyo na kuanza kumpiga kwa kutumia mawe hadi kufa,” alisema.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, Phillip Kalangi, alithibitsha kutokea kwa tukio hilo.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kagera Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa